News
Kina mama wajawazito na waliojifungua kwenye hospitali ya rufaa mjini Kilifi, wapokea zawadi kutoka Coco Fm
Uhaba wa wauguzi ni miongoni mwa changamoto ambazo zinatatiza shughuli za utoaji wa huduma za matibabu katika hospitali ya rufaa mjini Kilifi kaunti ya Kilifi.
Wakizungumza na Coco Fm, baadhi ya wauguzi wa hospitali ya rufaa Mjini Kilifi wakiongozwa na Nyadzua Pandau wamesema hali hiyo inawafanya kulazimika kufanya kazi kupita muda unaohitajika kwani idadi ya wagonjwa wanaohitaji matibabu ni kubwa kuliko ile ya wauguzi waliopo kwenye hospitali hiyo.
Vilevile, wametaja ukosefu wa dawa kwenye hospitali hiyo na kutoa wito kwa serikali ya Kaunti ya Kilifi kuhakikisha zinapatikana ili wagonjwa watibiwe bila changamoto zozote.
Aidha, wauguzi hao wameitaka serikali ya kitaifa pamoja na ya kaunti ya Kilifi kuwekeza zaidi katika kuimarisha huduma za matibabu na kukishukuru kituo cha COCO FM kwa kutoa zawadi kwa kina mama hospitalini humo jana wakati wa siku ya Kina duniani.
News
Mahakama ya Kilifi yawatupa gerezani washtakiwa zaidi ya 10
Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa washtakiwa zaidi ya 10 waliowasilishwa Mahakamani wakikabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwemo kesi za unajisi na makosa ya jinai.
Katika vikao vya Mahakama siku ya Jumatano tarehe 3 June 2026, Hakimu Ivy Wasike ametoa hukumu hizo kwa watuhumiwa hao huku wengine wakifungwa kwa zaidi ya miaka 30 gerezani.
Simon Ngala, Aliwali Ali Mwalimu, Christopher Buru, miongoni mwa wengine zaidi ya 10 walifikishwa katika Mahakama ya Kilifi na kuhukumiwa kufuatia mashtaka mbalimbali yanayowakabili ikiwemo mashtaka ya unajisi na makosa ya jinai.
Hakimu wa Mahakama ya Kilifi Ivy Wasike, alimhukumu kifungo cha miaka 30 gerezani Simon Ngala baada ya kupatikana na hatia ya kumnajisi mtoto wa miaka 13 kisha akamtorosha kwao kwa kipindi cha mwezi mzima.
Mwengine ni Aliwali Ali Mwalimu, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 25 kufuatia mashtaka ya kumpachika ujauzito mtoto wa miaka 13 licha ya kuomba msamaha Mahakamani.
Wakati wa kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisikitishwa na kukithiri kwa visa vya watoto kupotea na kisha kunajisiwa katika kaunti ya Kilifi.
Kiongozi wa mashtaka katika Mahakama hiyo Nancy Njeru alipinga vikali ombi lililowasilishwa Mahakama la kutaka washtakiwa wasamehewe, kwanin wengine walidai kwamba walishirika makosa hayo bila kukusudia, akisema hukumu hizo zitakuwa funzo kwa watu wenye hulka hizo katika jamii.
Mbali na hukumu za kesi za unajisi, Christopher Buru alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani akikabiliwa na mashtaka ya wizi baada ya kupatikana na hatia ya kutumia pesa za mlalamishi Saumu Nyevu aliyekuwa akimtumia pesa alipokuwa akifanya kazi katika milki za kiarabu, kosa lililomchukiza zaidi Hakimu Wasike.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Washukiwa 5 wa uhalifu wanazuiliwa na polisi Likoni
Maafisa wa polisi katika eneo bunge la Likoni kaunti ya Mombasa wanawazuiliwa washukiwa 5 wa uhalifu waliokamatwa katika oparesheni iliyofanyika maeneo ya Duduz na Bufallo siku ya Jumatatu tarehe mosi Juni 2026.
Washukiwa waliokamatwa ni Brian Musa mwenye umri wa miaka 24, Abubakar Mahasi wa umri wa miaka 20, Juma Kassim mwenye umri wa miaka 16, Omar Gobeko maarufu Mboga mwenye umri wa miaka 19 na Jackson Mwambu mwenye umri wa miaka 26.
Msako huo uliongozwa na mkuu wa kituo cha polisi cha Shelly Beach pamoja na kikosi cha maafisa wa polisi.
Maafisa wa Polisi wamesema mshukiwa Brian Musa anakabiliwa na tuhuma za maandalizi ya kutenda kosa la jinai, huku Ababakar Mahasi, Juma Kassim na Omar Gobeko wakihusishwa na tuhuma za wizi wa mabavu.
Mshukiwa mwengine Jackson Mwambu anahusishwa na tuhuma za kupatikana na mali ya serikali kinyume cha sheria.
Katika oparesheni hiyo, maafisa wa polisi walifanikiwa kupata vielelezo mbali mbali ikiwemo panga tatu pamoja na koti la jeshi la KDF.
Taarifa ya Joseph Jira


Thomaskombe
May 13, 2025 at 1:28 pm
Coco fm radio ina matangazo bora
Twaomba itufikie huku mitaani kweku
Magarini naviungani maana tuna hitaji matangazo na burudani
Na vipindi vya salamu