Connect with us

Uncategorized

Maafisa wa Kliniki watia saini mkataba wa kurejea kazini

Published

on

Baraza la magavana, bodi ya huduma za umma kaunti ya Mombasa pamoja na Muungano wa maafisa wa Kliniki nchini (KUCO), wametia saini mkataba wa makubaliano ya kurejea kazini. 

Mweyekiti wa kamati ya ukusanyaji wa rasilimali na ushirikiano katika baraza la magavana ambaye pia ni Gavana wa Nandi Stephen Sang, Mwenyekiti wa Bodi ya huduma za umma kaunti ya Mombasa Farida Abdallah, pamoja na viongozi wa Muungano wa maafisa wa Kliniki wameshuhudia kutiwa saini kwa mkataba huo.

Makubaliano hayo yamehitimisha rasmi mgomo wa kitaifa wa siku 36 wa maafisa wa kliniki, uliyokuwa umesitisha shughuli za utoaji wa huduma za afya katika vituo vya afya vya umma kote nchini.

Mchakato wa mashauriano, uliotegemea mazungumzo na ujenzi wa maridhiano, ulihitimishwa kwa ahadi ya Serikali za kaunti kutekeleza kikamilifu maazimio yaliyokubaliwa, ikiwemo kutiwa saini kwa mkataba wa makubaliano wa malipo nchini CBA, unaotarajiwa kufanyika Februari tarehe 2 mwaka huu.

Mpangilio wa kurejea kazini unafungua njia ya kurejelewa kwa huduma muhimu za afya na unaimarisha dhamira ya uongozi wa kaunti katika kuimarisha mifumo ya afya ya umma.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Uncategorized

Mshukiwa wa mauaji kuzuiliwa rumande kwa siku 7

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa rumande mshukiwa wa mauaji ya Ruth Ochieng’ mwenye umri wa miaka 60 kutoka kaunti ya Kisumu baada ya mshukiwa Evans Otieno kukamatwa katika Kanisa la Newlife Prayer Center lililoko eneo la Mavueni kaunti ya Kilifi.

Otieno alitiwa nguvuni na maafisa wa usalama alipokiri kwamba alitekeleza mauaji hayo mbele ya Mchungaji wa Kanisa hilo Ezekiel Odero, akitaka aombewe kama hatua moja wapo ya kutubu dhambi zake.

Hakimu wa Mahakama ya Kilifi Charles Obulutsa amesema Otieno atazuiliwa rumande kwa siku 7 ili kumuwezesha afisa wa polisi wa kituo cha polisi cha Seme mjini Kisumu anayechunguza kesi hiyo kufika Mahakamani.

Hakimu Obulutsa, ameeleza Mahakama kwamba wakati afisa huyo wa Polisi atakapofika katika Mahakama ya Kilifi atapewa idhini ya kumchukua mshukiwa ili afunguliwe mashtaka ya mauaji mjini Kisumu.

Awali Mahakama ilielezwa kwamba mwili wa mahehemu ulipatikana na kuthibitishwa kwamba alikuwa amenyongwa na uchunguzi zaidi ulikuwa unaendelea kabla ya mshukiwa kukamatwa katika maeneo ya Kanisa la Newlife Prayer Centre, eneo la Mavueni kaunti ya Kilifi.

Kesi hiyo itatajwa tena Februari 11 katika ili kuwakabidhi maafisa wa Polisi kutoka kaunti ya Kisumu mshtakiwa huyo.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Uncategorized

Wakenya wanaopata mshahara wa chini ya elfu 30 kuondolewa PAYE

Published

on

By

Waziri wa Fedha nchini John Mbadi amesema serikali inalenga kuwaondolea ushuru wa PAYE wakenya wanaopata mshahara wa chini ya shilingi elfu 30 kwa mwezi huku wale wanaopata mshahara wa shilingi elfu 30 hadi laki tano wakitozwa ushuru wa asilimia 25.

Waziri Mbadi alisema hatua hiyo inalenga zaidi ya wakenya milioni 1.5 na hivi karibuni atawasilisha mswada bungeni ili pendekezo hilo liangaziwe na sheria ya ushuru ifanyiwe marekebisho kabla ya kupitishwa kwa mswada wa fedha wa mwaka wa 2026.

Waziri Mbali aliyasema hayo wakati wa kikao cha kukusanya maoni ya umma katika kaunti ya Meru ambapo alikuwa amefanya kikao cha mazungumzo na Rais William Ruto na kuafikiana kuhusu pendekezo hilo.

Waziri huyo wa fedha nchini aliongeza kwamba mswada huo pia utajumuisha pendekezo la kupunguza ushuru wa PAYE kwa asilimia 5 kwa wakenya wanaopokea mshahara wa kati ya shilingi elfu 32,050 kwa mwezi hadi shilingi laki tano, akisema punguzo hilo la asilimia 5 litasaidia wakenya kumudu gharama ya maisha.

“Tumekubaliana na Rais kwamba wananchi wenye kipato cha chini wanapaswa kupata nafuu kwenye mishahra yao kwani idadi kubwa ya wananchi wanapitia hali ngumu ya maisha na hatua hii itasaidia wakenya wengi kuwa na pesa mfukoni. Sidhani kama kuna mbunge yeyote atapinga pendekezo hilo”, alisema Mbadi.

Waziri huyo wa fedha alishikilia kwamba hatua hiyo inalenga kupunguza mzingo wa ushuru kwa wakenya wa kipato cha chini na cha kati na kuwasaidia kujikimu katika kipindi hiki cha gharama ya juu ya maisha.

Kwa sasa kikomo cha ushuru wa PAYE kinaathiri wakenya wengi wenye kupokea mshahara wa kuanzia shilingi elfu 24, akisema wataalamu wamebaini kwamba kupunguzwa kwa ushuru kutachangia matumizi ya nyumbani kuwa ya usawa na kusaidia kuimarisha uchumi unaokabiliwa na mahitaji duni.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending