Connect with us

Business

Maandalizi ya maonyesho ya Kilimo Mombasa yaanza.

Published

on

Wafanyabiashara kutoka ndani na nje ya nchi wamehimizwa kushiriki kikamilifu kwenye maonyesho ya kilimo yatakayofanyika mwezi wa september mwaka 2025 katika uwanja wa maonyesho ya kilimo jijini Mombasa.

Mwenyekiti wa maandalizi ya maonyesho hayo eneo la pwani Henry Nyaga alisema hatua hiyo itawasalidia wakulima na wafanyabiashara kubadilishana maarifa na uzoefu katika nyanja ya kilimo-biashara.

Nyaga aidha alieleza kuwa mwaka huu 2025 kutakuwa na ushirika wa wadau wapya kutoka ndani na nje ya nchi.

Alidokeza kuwa masuala ya uchumi wa raslimali za bahari na maziwa yatapewa kipaumbele katika maonyesho hayo.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyibiashara wa mitumba eneo la Diani wafunga biashara zao

Published

on

By

Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Diani, kaunti ya Kwale, wamelazimika kufunga biashara zao kutokana na kudorora kwa shughuli za kibiashara katika kipindi hiki cha msimu wa watalii wachache na mvua zinazoendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.

Wafanyabiashara hao wanasema idadi ya wanunuzi imepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosababisha nguo nyingi kukosa soko.

Kulingana na wafanyibiashara hao wanategemea zaidi watalii wa ndani na nje  na kutokana na msimu huu kuwa uko uko chini wateja wamepungua hali inayofanya maisha kuwa mgumu.

Wanasema  wamelazimika kutupa baadhi ya nguo kwani  zimesalia sokoni kwa  muda mrefu hadi zingingine kuharibika, jambo ambalo limepelekea kupata hasara kubwa.

Aidha, wameongeza kuwa bei ya nguo za mitumba imeendelea kupanda ambapo wananunua ngunia moja kwa shilingi elfu 40 huku mauzo yakizidi kushuka.

“ Biashara imedorora sai kwani hakuna wateja ikizingatiwa kuwa tunategemea sana watalii na sasa hakuna wageni hata imetulazimu kutupa nguo kwani ngigi zimeharibika baada ya kukaa kwa mda mrefu bila kununuliwa”.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho

Published

on

By

Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.

Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.

Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.

Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.

Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.

“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending