News
Marekani yarusha makombora Iran, Trump akionya Tehran
Marekani imerusha mabomu kwenye maeneo ya Vinu vya Nyuklia vya Iran yanavyojumuisha Fordo na kuharibu kabisa maeneo hayo hatua ambayo huenda ikachangia vita zaidi ya kimataifa.
Rais wa Marekani Donald Trump alisema maeneo hayo yanayojumuisha Fordo, yalipigwa na makombora ya jeshi la Marekani huku Marekani ikijiunga na mashambulio ya Israel dhidi ya mpango wa Nyuklia wa Tehran.
Katika hatuba yake vya vyombo vya habari, Rais Trump alisema kwamba ni lazima Iran isitishe vita na kukumbatia amani iwapo wanataka vinu vyao vya Nyuklia kutorushiwa makombora.

Picha kwa hisani
“Tayari tumevuruga na kuharibu vinu vya Nyuklia vya Iran na bado tutaendelea kurusha makombora ya kasi zaidi na kuharibu vinu vyote vya Nyuklia vya Iran iwapo makao ya Tehran hayatasalimu amri”, alisema Rais Trump katika hotuba yake.
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya nje wa Iran Seyed Abbas Araghchi alilaani vikali shambulizi la Marekani na kusema kwamba ni shambulizi la kuchukiza na kwamba Tehran ina njia zote za kutetea uhuru wake.
“Matukio ya asubuhi ya leo ni ya kuchukiza na yatakuwa na matokeo ya milele. Kila Mwanachama wa Umoja wa Mataifa ni lazima ashtushwe na tabia hii hatari sana, isiyo ya kisheria bali ni tabia ya kihalifu,” alisema Seyed.
Seyed aliongeza kwamba Marekani ilifanya ukiukaji mkubwa wa Katiba ya Umoja wa Mataifa kama Mwanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Wajumbe wa bunge la Seneti wazuru kaunti ya Kilifi
Baadhi ya wajumbe wa bunge la Seneti chini ya mpango wa Seneti mashinani wamefanya ziara katika majengo ya bunge la kaunti ya Kilifi na kupokelewa na Karani wa bunge hilo Michael Ngala.
Wajumbe hao wa sekta mbalimbali wa bunge la Seneti wakiongozwa na Daniel Chania, wametathmini masuala mbalimbali ya bunge la kaunti ya Kilifi kama lina uwezo wa kuandaa ziara ijayo ya Seneti mashinani.
Seneti Mashinani ilianzishwa chini ya kifungu cha 126 ibara ya kwanza ya Katiba ya Kenya ya mwaka 2010, kinachoruhusu kikao cha bunge lolote kufanyika mahali popote ndani ya taifa la Kenya na kuanza wakati wowote kitakapopangwa na bunge.
Malengo ya vikao hivyo katika kaunti ni pamoja na kuhamasisha umma kuhusu kazi za bunge na Seneti, kuimarisha ushiriki wa umma katika shughuli za Seneti kwenye ngazi ya kaunti sawa na kutoa hamasa kwa wananchi kwa lengo la kuhimiza ushiriki umma katika utawala.

Baadhi ya wajumbe wa bunge la Seneti chini ya mpango wa Seneti mashinani wamefanya ziara katika majengo ya bunge la kaunti ya Kilifi
Bunge la Seneti limeanza maandalizi ya vikao vitakavyofanyika nje ya Nairobi, ambavyo vinatarajiwa kufanyika mwezi Septemba 2026.
Kaunti ya Kilifi ni miongoni mwa kaunti zilizoteuliwa kuwa kati ya zile zitazoandaa vikao hivyo kwa ajali ya umma kuwa na uelewa zaidi kuhusu shughuli za bunge hilo.
Wajumbe hao walikuwa na malengo pia ya kubaini upatikanaji wa miundombinu na huduma muhimu ili kuiwezesha Seneti kufanya uamuzi.
Kaunti nyingine zilizowahi kuandaa Seneti Mashinani ni pamoja na kaunti ya Uasin Gishu mwaka 2018, ikifuatiwa na kaunti ya Kitui mwaka 2019, kaunti ya Turkana mwaka 2023 na kaunti ya Busia mwaka 2025.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Sakata ya mafuta yaathiri sekta ya uchukuzi nchini
Huenda watumizi wa magari ya uchukuzi wa umma, wahudumu wa tuktuk na bodaboda wakalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na changamoto za ukosefu wa mafuta nchini na kuathiri zaidi shughuli za uchukuzi.
Hatua hii imetakana na changamoto za uhaba wa mafuta nchini baada ya kuibuka kwa sataka ya uagizaji wa mafuta ghushi kupitia bandari ya Mombasa.
Kulingana na serikali kupitia Wizara ya Kawi, sakata hiyo ya shilingi bilioni 12 ilikuwa imelata tani elfu 60 za mafuta ya petroli kinyume cha sheria pamoja na mipango ya serikali ya uagizaji mafuta wa serikali kwa serikali yaani G to G.
Sakata hii imepelekea Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya kudhibiti kawi na bei za mafuta nchini EPRA Daniel Kiptoo, Katibu katika Idara ya petroli nchini Mohammed Liban na mkurugenzi wa Kampuni ya Kenya Pipeline Joe Sang kujiuzulu.
Kujiuluzu kwao kumetokana na kukamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI, kwa ushirikiano na Tume ya maadili na kupambana na ufisadi nchini EACC baada ya kutilia shaka zabuni iliyopewa kampuni binafsi ya One Petroleum Limited inayomilikwa na mfanyibiashara mashuhuri jijini Mombasa.

Wahudumu wa sekta ya bodaboda wakikabiliwa na changamoto za uhaba wa mafuta ya Petroli
Siku ya Jumanne, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandanyi alifanya kikao na wakurugenzi wa kampuni za mafuta nchini na kuagiza shehena ya mafuta katika bandari ya Mombasa kurejeshwa kwani serikali haitambua shehena hiyo.
“Wahusika wa sakata hiyo walikuwa na njama ya kuongeza bei ya mafuta nchini kwa shilingi 14 zaidi kwa lita wakitumia nafasi ya vita vinavyoendelea kati ya Iran na Marekani na Israel, hiyo hatuta kubali”, alisema Wandayi.
Hatua hiyo ilikuwa inalenga pia kukwepa mpango wa serikali wa uagizaji mafuta kutoka mataifa ya miliki za kiarabu wa serikali kwa serikali yaani G to Go, akisema wahusika wa sakata ya ufisadi ni lazima wachukuliwe hatua.
Itakumbukwa kwamba rais William Ruto hivi majuzi alidokeza kwamba wahusika wote wa sakata ya ufisadi kwenye sekta ya mafuta watachukuliwa hatua, akishililia kwamba serikali haitakubali ufisadi nchini, huku akikosa kuweka wazi hatma ya maafisa hao wakuu wa serikali.
“Hawa walaghai wa mambo ya mafuta watakipata, hawaweze kuhepa kwa sababu haiwezekani katika taifa letu la Kenya watu wanaone tuko na shida ya mashariki ya kati wanakuja kukoroga shida nyengine hapa Kenya, serikali itakabiliana kikamilifu na wafisadi”, alisema Rais Ruto.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

