Connect with us

News

Mashahidi zaidi wajitokeza dhidi ya Mackenzie

Published

on

Kesi dhidi ya mhubiri tata Paul Mackenzie na washukiwa wenzake 38 kuhusu ukatili na ukiukaji wa haki za watoto inaendelea kusikizwa katika mahakama ya watoto ya Tononoka, Mombasa mbele ya hakimu mkuu Nelly Chepchirchir.

Shahidi wa 43, Sajenti mwandamizi Joseph Yator, alieleza jinsi mtoto aliyenusurika kutoka Shakahola alivyoripoti kuwa watoto wawili walifunikwa nyuso na mama zao hadi kufariki baada ya kushindwa kufa kwa kufunga.

Yator alisema alipewa amri ya mahakama kufukua miili hiyo ili kubaini chanzo cha vifo hivyo, lakini baada ya Mackenzie kuachiliwa kwa dhamana ya polisi, alikuta makaburi hayo yakiwa matupu.

Aliongeza kuwa mwili mmoja kati ya hiyo miwili ulipatikana kwenye  kaburi tofauti na kupelekwa kwa vipimo vya DNA, ambapo matokeo yalionyesha kufanana kwa asilimia 99 na ndugu wa familia hiyo.

Shahidi wa 44, Julius Kiprotich, alisimulia jinsi mkewe, Alice Kawira, aliyefuata mafundisho ya Mackenzie, alivyochoma vitabu na sare za shule za watoto wao, na pia kumtoa mamake hospitalini na kutupa dawa zake, akidai matibabu ni ushetani.

Kiprotich alitoa ushahidi wa kusikitisha akieleza jinsi mkeke na wafuasi wengine wa kanisa la Good News International walivyosherehekea kifo cha mtoto wao wa pili badala ya kuomboleza, baada ya mkewe kushindwa kumpeleka mtoto hospitalini.

Alieleza mahakama jinsi mkewe alivyomtoa mtoto kwa siri kutoka shule na kuhamia Shakahola na kisha kukatiza mawasiliano.

Mama yake Julius Kiprotich, Bi. Hellena, pia alithibitisha ushahidi  wa mwanawe kwa kueleza kuwa Alice Kawira na Julius walikuwa wanandoa na walikuwa na watoto wawili, ushahidi wake pia uliunga mkono madai ya Julius kwamba Alice Kawira alimtoa mtoto wao shuleni Eldoret na kuhamia Malindi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending