Connect with us

News

Mgombea Urais 2027 Robert Watene Aahidi Kukabili Ufisadi

Published

on

Mgombea wadhifa wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 Robert Watene anasema taifa litanawiri zaidi na kuendelea iwapo wananchi watahakikishiwa usalama wa chakula.

Watene alisema swala hilo ni miongoni mwa mambo muhimu atakayoyapa kipambele katika manifesto yake.

Vile vile mgombea huyo alisema wananchi wanafaa kuhakikishiwa upatikanaji rahisi wa maji safi pamoja na mfumo bora wa huduma za afya kwa wote.

Alidokeza kuwa huduma za afya iwapo zitapelekwa karibu na wananchi, mambo mengi yataepukika ikiwepo gharama ya usafiri na mda kupotezwa miongoni mwa wananchi.

“Tuko na shida ya chakula cha tumbo na utaskia mara hakuna unga, hiki chakula tunataka tuangalie ni vipi tunaweza kuwezesha wakenya wote wawe wakipata chakula kila wakati, jambo la pili ni maji safi, unajua ni watu wangapi wanateseka na maji, kunawengine hata kupata hayo maji wameenda kilomita nyingi kupata maji, mabo ya matibabu tumeyafanya yawe magumu sana kwa wananchi wengi,na sio sawa, saa hii ukienda hapa hospitali kuu utapata foleni ndefu mtu anakwambia nimekuwa hapa siku mbili sijahudumiwa na daktari, mbona tufanye hivyo”,alisema Watene.

Wakati huo huo aliahidi kuangazia sekta ya elimu na kuifanya ya elimu iwe ya bila malipo nchini, kuboresha usalama wa nchi, kukabiliana na ufisadi pamoja na kutokomeza ukabila.

“Kuna mambo na masomo hatuko sawa hata kidogo, tunatakikana masomo yawe haki ya kila mtu, na kutoka gredi ya kwanza hadi chuo kikuu serikali igharamie hayo masomo, nafasi za kazi watu wengi hawana kazi ya kufanya na sio eti hawataki kufanya kazi, hakuna nafasi za kazi, kuna mnyama mmoja anaitwa ufisadi lakini napenda nimgawanye mara mbili, wakwanza anaitwa wizi wa mali ya umma, halafu mwengine ni mambo ya hongo na vitu vidogo vidogo, ukabila ni kitu kibaya sana unaweza fanya ujichukie, unawezafanya mpigane, muuane na tushaona yakifanyika, hii lazima tumalize”,alisistiza mgombe huyo.

Mwanaharakati huyo atakuwa miongoni mwa vigogo wa siasa ambao watapambana kwenye uchaguzi mkuu ujao ambapo kwa sasa baadhi yao wameanza kuuza sera zao kwa wakenya.

Taarifa na Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending