Connect with us

News

Mkasa wa moto katika shule ya Utumishi Girls Academy wasababisha vifo 16

Published

on

Serikali imethibitisha kwamba wanafunzi 16 wa shule ya upili ya wasichana ya Utumishi Girls Academy eneo la Gilgil kaunti ya Nakuru wameaga dunia na wengini 79 wakajeruhiwa kufuatia mkasa wa moto ulitokea katika shule hiyo.

Waziri wa Elimu nchini Julius Migos amesema shule hiyo ilikuwa na wanafunzi 808 wakati wa mkasa huo wa usiku wa kuamkia siku ya Alhamis 28, Mei 2026, ambapo bweni moja la wanafunzi wa shule hiyo lilishika moto na kuteketea.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kutembelea shule hiyo, Waziri Migos alisema kati ya wanafunzi 79 waliyopata majeraha na kukimbizwa hospitalini, 71 kati yao walipokea matibabu na kuruhusiwa kuondoka na wazazi wao, wanafunzi wengine 7 wakiendelea kulazwa hospitalini.

Migos hata hivyo ameonya kuchukuliwa kwa hatua kali za kisheria kwa mtu yeyote atakayepatikana amehusika katika mkasa huo wa moto kwenye shule hiyo ya Utumishi Girls Academy huku akiagiza kufungwa kwa shule hiyo kwa muda.

“Ningependa kusema kwamba sote tunajua kwamba mkasa huu umesababishwa na moto lakini uchunguzi ukikamilika na tubaini kwamba kuna watu walihusika iwe ni wanafunzi ama mtu binafsi serikali itamchukulia hatua kali zaidi”, alisema Migos

Naye Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen aliwataka wananchi kuwa utulivu na kuepuka kusambaza taarifa zisizo na uhakika mitandaoni kwani maafisa wa usalama bado wanaendelea na uchunguzi.

“Tunawataka wakenya wawe watulivu wakati uchunguzi ukiendelea na tutaeleza kila kitu baada ya kupata taarifa kamilifu kutoka kwa maafisa wetu wa upelelezi lakini sio vizuri kuweka mambo kwa mitandao na haujapata taarifa kamili,”alisema Murkomen.

Hata hivyo wazazi waliyofika katika shule hiyo wamependezeka mabweni yote katika shule mbalimbali nchini kuweka madirisha makubwa na milango mingi ili kuokoa maisha ya wanafunzi wakati wa mikasa ya moto sawa na sheria zilizowekwa na serikali kuhakikisha zinatekelezwa kikamilifu.

Maafisa wa Idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI wamesema tayari wameanzisha uchunguzi ili kubaini chanzo cha mkasa huo wa moto katika shule hiyo ya upili ya wasichana ya Utumishi Girls Academy huko Gilgil kaunti ya Nakuru.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Baraza la Jamii ya Sekuye lalamikia uchimbaji wa madini kiholela

Published

on

By

Baraza la Wazee wa jamii ya Sekuye eneo la Moyale kaunti ya Marsabit limejitokeza na kulalamikia kuharibiwa kwa mazingira ya maeneo yao hasa katika kijiji cha Dabel kutokana na uchimbaji madini kiholela.

Wazee hao wamewalaumu viongozi wao ikiwemo serikali ya kaunti kwa kulinyamazia suala hilo huku wakaazi wakiendelea kunyanyaswa raslimali zao.

Baraza hilo, chini ya Katibu wake mkuu Haji Hassan Tepo, limedai kwamba uchimbaji huo wa madini kiholela, unyakuzi wa ardhi, unyanyasaji wa jamii umechangiwa na baadhi ya wawekezaji kutoka taifa Jirani la Somalia na Ethiopia ambao hawana vibali halali.

Hassan aliimtaka serikali kupitia Waziri wa madini nchini Hassan Ali Joho kuingilia kati suala hilo na kuhakikisha uchumbaji wa madini katika kijiji cha Dabel unasitishwa kwani wawekezaji zaidi ya 20 wamebuni makundi na kuendelea kuwanyanyasa wenyeji.

Hassan aliweka wazi kwamba baraza hilo pamoja na jamii ya Sekuye linapinga mpango huo na kusisitisha kwamba hawatakubali ardhi yao wanayoitegemea kwa shughuli mbalimbali kutumika vibaya.

Naibu Mwenyekiti wa baraza hilo Abdukadir Dilo alisema hali hiyo imewasabibishia hasara kwani mifugo imeangamia, uchumi wa kijiji hicho ukididimia zaidi na akamtaka rais Ruto kuingilia kati kwani licha ya Waziri Murkomen kufunga uchumbaji kufuatia utovu wa usalama bado wawekezaji kutoka Ethiopia na Somali wamekuwa wakiendeleza mpango huo.

Wazee hao hata hivyo walisisitiza kwamba hawatakubali kuachilia ardhi yao kunyakuliwa na watu wanaodai kuwa wawekezaji ilhali vijana wa eneo hilo hawana kazi, huku wanafunzi wakiacha shule na zaidi ya akina mama 22 wakiachwa na wanaume zao kufuatia suala hilo katika kijiji cha Dabel.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Murkomen ahimiza ushirikiano wa pamoja na wadau wa masuala ya ubaharia

Published

on

By

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen, ametoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya washirika na wadau ili kuimarisha usalama wa baharini na maziwa makuu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa kongamano la kamati ya uongozi wa Jukwaa la ushirikiano wa taarifa ya kanda ya Indo-Pasifiki (IORIS) lililofanyika mjini Mombasa, Waziri huyo alisisitiza kuwa ushirikiano wa mapema ni muhimu katika kukabiliana na vitisho vinavyoibuka vya usalama wa baharini.

“Ushirikiano wa mapema na muhimu katika kulinda usalama wetu wa baharini,” alisema Murkomen.

Kongamano hilo la siku tatu linaandaliwa kwa pamoja na huduma ya Walinzi wa Pwani ya Kenya (KCGS) pamoja na mradi wa njia muhimu za baharini wa Indo-Pasifiki unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU-CRIMARIO), ukiwaleta pamoja wadau wa usalama wa baharini..

Mradi wa EU-CRIMARIO umeundwa kuimarisha usalama na ulinzi wa baharini kupitia kuboreshwa kwa ushirikiano wa taarifa na uratibu wa operesheni.

Kongamano la siku tatu la kamati ya uongozi la Jukwaa la ushirikiano wa taarifa ya kanda ya Indo-Pasifiki (IORIS), Mombasa

Mpango wake mkuu, IORIS, ni jukwaa salama na lisiloegemea upande wowote linalotumia mtandao, unaounganisha zaidi ya mashirika 150 kutoka nchi 70, na kuwezesha uratibu wa operesheni za baharini kwa wakati halisi.

Kauli za Murkomen ilijiri kufuatia tangazo la Rais William Ruto kwamba kampuni ya usafiri wa baharini ya Norway, Wilhelmsen, itaajiri mabaharia 1,000 kutoka Kenya, baada ya mazungumzo na kampuni hiyo.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mkurugenzi wa EU-CRIMARIO Martin Cauchi Inglott, Mkurugenzi mkuu wa huduma ya walinzi wa Pwani ya Kenya Bruno Shioso, Naibu mkuu wa ujumbe wa umoja wa Ulaya nchini Kenya Ondrej Simek, pamoja na washkadau wengine.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending