Business
Muungano wa bodi za leseni za vileo wapinga sera ya NACADA
Muungano wa bodi za kudhibiti na kutoa leseni za vileo nchini umepinga vikali pendekezo la Sera ya Mwaka 2025 ya Mamlaka ya Kudhibiti Matumizi ya Pombe na Dawa za Kulevya (NACADA), wakidai kuwa linaenda kinyume na ugatuzi na kuondoa mamlaka ya kikatiba ya serikali za kaunti katika usimamizi wa biashara ya vileo.
Wakizungumza mjini Diani kaunti ya Kwale, wanachama wa Muungano huo wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Julius Owino, walisisitiza kuwa serikali za kaunti ndizo zenye jukumu la kisheria na kikatiba la kutoa leseni, kusimamia, na kutekeleza sheria zinazohusu uuzaji wa pombe.
“Sera hii ya NACADA ni jaribio la kuingilia majukumu ya kaunti na itaathiri mapato ya serikali za kaunti, kaunti lazima zisalie na mamlaka kamili ya kusimamia biashara ya vileo kama ilivyowekwa katika Katiba,” alisema Owino.
Owino pia aliitaka NACADA kushirikiana na kaunti kwa njia ya mashauriano badala ya kujaribu kuchukua majukumu yao, akiongeza kuwa ushirikiano thabiti ndio utaleta mafanikio katika udhibiti wa pombe na dawa za kulevya.
Kauli yake iliungwa mkono na Richard Osongo, Mwenyekiti wa wamiliki wa baa katika kaunti ya Kwale, ambaye alitoa onyo kali dhidi ya kile alichokiita “unyanyasaji wa mamlaka za kaunti na NACADA.”
Muungano huo ulieleza kuwa utatoa mapendekezo rasmi kwa serikali ya kitaifa na kuhimiza mjadala wa wazi kabla ya utekelezaji wowote wa sera hiyo mpya.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
Business
Wafanyibiashara wa mitumba eneo la Diani wafunga biashara zao
Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Diani, kaunti ya Kwale, wamelazimika kufunga biashara zao kutokana na kudorora kwa shughuli za kibiashara katika kipindi hiki cha msimu wa watalii wachache na mvua zinazoendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.
Wafanyabiashara hao wanasema idadi ya wanunuzi imepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosababisha nguo nyingi kukosa soko.
Kulingana na wafanyibiashara hao wanategemea zaidi watalii wa ndani na nje na kutokana na msimu huu kuwa uko uko chini wateja wamepungua hali inayofanya maisha kuwa mgumu.
Wanasema wamelazimika kutupa baadhi ya nguo kwani zimesalia sokoni kwa muda mrefu hadi zingingine kuharibika, jambo ambalo limepelekea kupata hasara kubwa.
Aidha, wameongeza kuwa bei ya nguo za mitumba imeendelea kupanda ambapo wananunua ngunia moja kwa shilingi elfu 40 huku mauzo yakizidi kushuka.
“ Biashara imedorora sai kwani hakuna wateja ikizingatiwa kuwa tunategemea sana watalii na sasa hakuna wageni hata imetulazimu kutupa nguo kwani ngigi zimeharibika baada ya kukaa kwa mda mrefu bila kununuliwa”.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho
Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.
Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.
Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.
Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.
Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.
“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

