Connect with us

Business

Mvua Yaua Soko la Mitumba Mariakani, Wateja Wapungua

Published

on

Wafanyabiashara wa kuuza mitumba katika soko la Mariakani kaunti ya Kilifi wamelalamikia kupungua kwa biashara hiyo hasa musimu huu wa Mvua.

Akiongea na mwahabari wetu, Mwenyekiti wa soko hilo Mwasingo Ngura amesema kwamba wateja wengi kwa sasa wameingia kilimo hali inayopelekea ukosefu wa wateja kwenye soko hilo.

Kiongozi huyo wa Soko hata hivyo amesema kwamba wanaamini biashara hiyo itaboreka baada ya msimu huu wa mvua kumalizika.

Wakati huo huo Ngura ameendelea kuilaumu serikali ya kaunti ya Kilifi kwa madai ya kukosa kutambua wafanyabiashara wa soko hilo katika kuboresha soko hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Biashara ya Mananasi yakabiliwa na changamoto Kilifi

Published

on

By

Wafanyibiashara kuuza matunda aina ya Nanasi kaunti ya Kilifi wanasema biashara ya matunda hayo inazidi kudorora msimu huu ikilinganishwa na msimu uliopita.

Kulingana na wafanyibiashara hao, matunda ya Mananasi hayapatikana kwa urahisi sokoni kutokana na mabadiliko ya hali ya angani licha ya biashara ya matunda hayo kuwa na thamani kubwa katika soko la Pwani na taifa.

Wakiongozwa na Japhet Khambi, wafanyibiashara hao walisema kwa sasa wanategemea matunda hayo kutoka nje ya nchi hasa taifa la Uganda ambapo uagizaji wa matunda hayo umekuwa ghali mno.

Katika suala la usafirishaji wa bidhaa hiyo katika soko la kaunti ya Kilifi kutoka taifa hilo jirani la Afrika Mashariki, wafanyibiashara hao walisema ghamara ya usafiri uko juu mno hali ilichangia bei ya bidhaa hizo kuongezeka mara dufu.

“Hii mambo ya gharama ya usafirishaji na uhaba wa matunda hayo bei ya bidhaa hiyo imepanda kwa kiwango kikubwa, alieleza Khambi.

Wafanyibiashara wa matunda ya Mananasi walisema Nanasi ambalo lilikuwa Linanunuliwa kwa shilingi 100 sasa tunda hilo limepanda bei na kuuzwa kwa shilingi 250.

“ Tulikuwa tunanunua Mananasi kutoka eneo la Chakama katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kwa bei nafuu lakini kwa sasa hayapatikani na kutulazimu kuangiza matunda kutoka Uganda.”, alisema Khambi.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Bei za mafuta kuongezeka katikati ya mwezi aprili

Published

on

By

Kenya sasa inakabiliwa na hatari ya kupanda kwa bei za mafuta, huku mgogoro unaoendelea mashariki ya Kati ukianza kuathiri bei nchini.

Serikali sasa imeonya kuwa kufikia katikati ya mwezi Aprili, bei za mafuta huenda zikapanda ikionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta kwa sasa haliwezi kuepukika kufuatia kupanda kwa bei za mafuta kimataifa.

Waziri wa hazina kuu ya kitaifa John Mbadi aliwahakikishia wakenya kuwa hakuna cha kuhofia kwani wameweka mikakati kupunguza athari zake.

Ili kupunguza athari za bei za mafuta kuongezeka, serikali ilisema itatumia shilingi bilioni 17 kutoka mfuko wa ada ya uwekezaji wa mafuta kusaidia kudhibiti bei kwa mda wa miezi 3 ijayo.

Kwa sasa serikali inasema kuna akiba ya kutosha ya mafuta na shehena zaidi zinatarajiwa nchini hivi karibuni.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending