News
Serikali yaonya wakenya dhidi ya maandamano
Serikali imewaonya wakenya hasa Vijana wa Gen Z kutokubali kushurutishwa na Wanasiasa na kushiriki maandamano ya kupinga kupanda kwa bei ya mafuta nchini.
Msemaji wa serikali Isaac Mwaura, aliwataka vijana kutokubali kushiriki maandamano ya siku ya Jumanne Aprili 21, akisema yatachangia kuharibika zaidi kwa uchumi wa taifa.
Katika kikao na Wanahabari jijini Nairobi, Mwaura alisema maandamano sio suluhu la kutatua changamoto zinazoshuhudiwa nchini bali yatachangia hasara kwa taifa ambalo linakuwa kiuchumi na maendeleo, akisisitiza haja ya wakenya kutafuta njia mbadala za kuwasilisha lalama zao na wala sio kushiriki maandamano.
Mwaura alisema maandamano yaliofanyika mwezi Juni mwaka 2024, yalichangia taifa kupata hasara ya shilingi bilioni 6, kulingana na takwimu za Mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini KRA, akiwataka wakenya kujitenga na maandamano hayo.
“Maandamano ya Juni mwaka wa 2024, alisababisha taifa kupata harasa ya zaidi ya shilingi bilioni 6 kwa hivyo haitakuwa bora kwa wanasiasa kuwatumia vijana vibaya kuharibu mali ya umma, hivyo basi wanasiasa wafanye mipango ya kuwatafutia kazi vijana”, alisema Mwaura.
Maandamano hayo yanalenga kuishinikiza serikali kupunguza bei ya mafuta nchini licha ya taifa kukumbwa na msukosuko wa changamoto za mafuta yaliochangiwa na sakata ya ufisadi ya uagizaji mafuta pamoja na mgogoro wa vita nchini Iran.
Vijana wa kizazi cha Gen Z, wamekuwa wakiikosoa serikali kutokana na kupanda kwa gharama ya maisha, tangu mwaka wa 2024 huku maandamano ya mara kwa mara nchini yakishuhudiwa katika baadhi ya maeneo, wakenya wakilalamikia kunyanyaswa na serikali.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Wakenya waonywa dhidi ya kuchipuka kwa magonjwa msimu wa mvua
Wizara ya Afya nchini imewarai wakenya kuchukua tahadhari ya mapema msimu huu wa mvua na kutibu maji wanayotumia kila siku ili kuepuka kukumbwa na magonjwa mbalimbali.
Katibu katika Idara hiyo Mary Muthoni, alisema baadhi ya maeneo yanashuhudia mvua nyingi na huenda ikaathiri wananchi iwapo hawatakuwa maniki dhidi ya kujikinga na magonjwa.
Alisema mara nyingi magonjwa wengine huchangiwa na mazingira machafu, na maji yaliochanganyika na maji taka, akisisitiza haja ya wananchi kuwa makini na kuhakikisha wanachamsha maji ya kunywa kwa usalama wao.
Katibu huyo alisema watu wengi wamekuwa na hulka ya kutumia maji ya visima na mabwawa na mara nyingi huwa na chembechembe ya viini, akisisitiza haja ya wananchi kuchukua tahadhari ya kutibu maji ama kuchemsha maji ya kunywa kabla ya kuyatumia ili kuepuka maambukizi ya maradhi mbalimbali.
Akizungumza katika kaunti ya Nyeri, Muthoni aliwarai wananchi kutopuuza tahadhari hiyo na kuhakikisha wanalinda afya zao.
“Kuna athari ya kuchupuka kwa magonjwa mbalimbali kama yale ya kuendesha kutokana na uchafuzi wa mazingira na utumizi wa maji ambayo hajatibiwa ama kuchemshwa, kwa hivyo langu ni kuwahimiza wananchi wachukue tahadhari ya mapema hasa msimu huu wa mvua ili kuepuka magonjwa”, alisema Muthoni.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Jubilee yaunga mkono maandamano ya kupinga bei ya mafuta
Kufuatia sakata ya uagizaji wa mafuta ghushi nchini, sasa Muungano wa upinzani umetishia kufanya maandamano kuanzia wiki ijayo.
Mwenyekiti wa kitaifa wa Chama cha Jubilee Vincent Kemosi, alisema maandamano hayo yanalenga kushinikiza kupunguzwa kwa bei ya mafuta nchini, akimshtumu Rais William Ruto kwa kuchangia mahangaiko wakenya.
Katika kikao na Wanahabari mjini Kilifi kaunti ya Kilifi baada ya kufanya kifanya kikao na viongozi wa chama hicho kanda ya Pwani, Kemosi aliikosoa serikali, akisema wakenya wamechoka kudanganywa na serikali iliyofeli kutekeleza ahadi zake.
“Serikali imeonyesha kushindwa kutatua suala la mafuta na imeonyesha wazi kwamba imefeli, huezi badilisha ushuru wa mafuta baada ya wananchi kulalamika mbona hakufanya hivyo tangu mwanzo, wakenya wamechoka”, alisema Kemosi.
Kemosi, amepinga mpango wa kugawa maeneo kisiasa yaani Zoning, akisema Viongozi wa Chama cha Jubilee watazingatia haki na usawa pamoja na kuandaa uchaguzi wa mashinani wa viongozi wa chama hicho, kauli iliyoungwa mkono na Mwenyekiti wa chama hicho kaunti ya Kilifi Anthony Kingi.
“Katika ya Kenya haijasema mambo ya Zoning, kila mtu ana haki ya kupigania wadhfa anataka, na sisi kama Chama cha Jubilee hatuingi mkono mambo ya zoning, tutahakikisha uchaguzi unafanyika mashinani kwa haki na uwazi”aliongeza Kemosi.

Viongozi wa Chama cha Jubilee wakiongozwa na Mwenyekiti wa kitaifa wa Chama hicho wafanya mkutano wa kuimarisha chama mashinani, Kilifi
Viongozi hao pia waliwarai wananchi kutathmini viongozi wao na kujiunga na vyama vinavyozingatia haki na usawa, wakisisitiza kuunga mkono upinzani.
Katika swala la raslimali, viongozi hao wameshtumu kutengwa kwa raslimali za Pwani hasa zao la mzani na mkorosho, wakisema wakati umefika kwa mpwani kutambulika na raslimali zake kuthaminiwa.
“Zao la Mnazi na Mkorosho ambayo ndio raslimali ya mpwani imetengwa tangu taifa ipate uhuru ndio sisi tunasema ni lazima raslimali ya mpwani pia nayo itambulike kikamilifu”, alisema Garama.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi.

