Connect with us

News

Serikali yaonya wakenya dhidi ya maandamano

Published

on

Serikali imewaonya wakenya hasa Vijana wa Gen Z kutokubali kushurutishwa na Wanasiasa na kushiriki maandamano ya kupinga kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Msemaji wa serikali Isaac Mwaura, aliwataka vijana kutokubali kushiriki maandamano ya siku ya Jumanne Aprili 21, akisema yatachangia kuharibika zaidi kwa uchumi wa taifa.

Katika kikao na Wanahabari jijini Nairobi, Mwaura alisema maandamano sio suluhu la kutatua changamoto zinazoshuhudiwa nchini bali yatachangia hasara kwa taifa ambalo linakuwa kiuchumi na maendeleo, akisisitiza haja ya wakenya kutafuta njia mbadala za kuwasilisha lalama zao na wala sio kushiriki maandamano.

Mwaura alisema maandamano yaliofanyika mwezi Juni mwaka 2024, yalichangia taifa kupata hasara ya shilingi bilioni 6, kulingana na takwimu za Mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini KRA, akiwataka wakenya kujitenga na maandamano hayo.

“Maandamano ya Juni mwaka wa 2024, alisababisha taifa kupata harasa ya zaidi ya shilingi bilioni 6 kwa hivyo haitakuwa bora kwa wanasiasa kuwatumia vijana vibaya kuharibu mali ya umma, hivyo basi wanasiasa wafanye mipango ya kuwatafutia kazi vijana”, alisema Mwaura.

Maandamano hayo yanalenga kuishinikiza serikali kupunguza bei ya mafuta nchini licha ya taifa kukumbwa na msukosuko wa changamoto za mafuta yaliochangiwa na sakata ya ufisadi ya uagizaji mafuta pamoja na mgogoro wa vita nchini Iran.

Vijana wa kizazi cha Gen Z, wamekuwa wakiikosoa serikali kutokana na kupanda kwa gharama ya maisha, tangu mwaka wa 2024 huku maandamano ya mara kwa mara nchini yakishuhudiwa katika baadhi ya maeneo, wakenya wakilalamikia kunyanyaswa na serikali.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending