Connect with us

News

Serikali yaonya wakenya dhidi ya maandamano

Published

on

Serikali imewaonya wakenya hasa Vijana wa Gen Z kutokubali kushurutishwa na Wanasiasa na kushiriki maandamano ya kupinga kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Msemaji wa serikali Isaac Mwaura, aliwataka vijana kutokubali kushiriki maandamano ya siku ya Jumanne Aprili 21, akisema yatachangia kuharibika zaidi kwa uchumi wa taifa.

Katika kikao na Wanahabari jijini Nairobi, Mwaura alisema maandamano sio suluhu la kutatua changamoto zinazoshuhudiwa nchini bali yatachangia hasara kwa taifa ambalo linakuwa kiuchumi na maendeleo, akisisitiza haja ya wakenya kutafuta njia mbadala za kuwasilisha lalama zao na wala sio kushiriki maandamano.

Mwaura alisema maandamano yaliofanyika mwezi Juni mwaka 2024, yalichangia taifa kupata hasara ya shilingi bilioni 6, kulingana na takwimu za Mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini KRA, akiwataka wakenya kujitenga na maandamano hayo.

“Maandamano ya Juni mwaka wa 2024, alisababisha taifa kupata harasa ya zaidi ya shilingi bilioni 6 kwa hivyo haitakuwa bora kwa wanasiasa kuwatumia vijana vibaya kuharibu mali ya umma, hivyo basi wanasiasa wafanye mipango ya kuwatafutia kazi vijana”, alisema Mwaura.

Maandamano hayo yanalenga kuishinikiza serikali kupunguza bei ya mafuta nchini licha ya taifa kukumbwa na msukosuko wa changamoto za mafuta yaliochangiwa na sakata ya ufisadi ya uagizaji mafuta pamoja na mgogoro wa vita nchini Iran.

Vijana wa kizazi cha Gen Z, wamekuwa wakiikosoa serikali kutokana na kupanda kwa gharama ya maisha, tangu mwaka wa 2024 huku maandamano ya mara kwa mara nchini yakishuhudiwa katika baadhi ya maeneo, wakenya wakilalamikia kunyanyaswa na serikali.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

IEBC: Hatutaongeza muda wa usajili wa wapiga kura

Published

on

By

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imesema haitaongeza mda wa usajili wa wapiga kura kote nchini.

Makamishna wa Tume hiyo wameshikilia kwamba wakati muda huo uliyotengwa utakapokamilika, basi itakuwa ndio mwisho wa zoezi hilo.

Tume hiyo ilisema japo tayari imesajili zaidi ya wakenya milioni moja licha ya kukadiria kusajili idadi ya wakenya milioni 6.5, juhudi hizo zimeonekana kutofikia malengo hitajika.

IEBC ilikuwa imetangaza kusajili wapiga kura wapya milioni 6.5 ikilenga vijana wa Gen Z katika zoezi hilo huku vijana wenyewe wakizindua mpango wa NIKO KADI kama mbinu mbadala ya kusajili idadi kubwa zaidi ya wapiga kura kote nchini, bado juhudi hizo zimeokena kutofikia malengo ya IEBC.

Kamishna wa IEBC Hassan Noor Hassan aliwarai vijana wa kizazi cha Gen Z kutopuuza zoezi hilo na kutumia muda uliyosalia wa kipindi cha wiki moja kujisajili kama wapiga kura, akisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha wakenya wanapata fursa ya kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu ujao.

Noor alisema vifaa vya usajili wa wapiga kura vya kieletroniki ama KIEMS KIT vimewasilishwa hadi mashinani na maafisa wa Tume hiyo wanafanya kila juhudi kuhakikisha wakenya wanaojitokeza kwa usajili huo wanasajili.

“Tumepeleka vifaa vya kusajili wapiga kura wapya hadi mashinani vya KIEMS KIT, na tuko na matumaini makubwa kwamba tutafikia idadi tunayolenga ya wapiga kura wapya milioni 6.5, na tunawarai wakenya kujitokeza kwa wingi na kujisajili kwa kutumia muda uliyosalia wa wiki moja”, alisema Noor.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Wakenya waonywa dhidi ya kuchipuka kwa magonjwa msimu wa mvua

Published

on

By

Wizara ya Afya nchini imewarai wakenya kuchukua tahadhari ya mapema msimu huu wa mvua na kutibu maji wanayotumia kila siku ili kuepuka kukumbwa na magonjwa mbalimbali.

Katibu katika Idara hiyo Mary Muthoni, alisema baadhi ya maeneo yanashuhudia mvua nyingi na huenda ikaathiri wananchi iwapo hawatakuwa maniki dhidi ya kujikinga na magonjwa.

Alisema mara nyingi magonjwa wengine huchangiwa na mazingira machafu, na maji yaliochanganyika na maji taka, akisisitiza haja ya wananchi kuwa makini na kuhakikisha wanachamsha maji ya kunywa kwa usalama wao.

Katibu huyo alisema watu wengi wamekuwa na hulka ya kutumia maji ya visima na mabwawa na mara nyingi huwa na chembechembe ya viini, akisisitiza haja ya wananchi kuchukua tahadhari ya kutibu maji ama kuchemsha maji ya kunywa kabla ya kuyatumia ili kuepuka maambukizi ya maradhi mbalimbali.

Akizungumza katika kaunti ya Nyeri, Muthoni aliwarai wananchi kutopuuza tahadhari hiyo na kuhakikisha wanalinda afya zao.

“Kuna athari ya kuchupuka kwa magonjwa mbalimbali kama yale ya kuendesha kutokana na uchafuzi wa mazingira na utumizi wa maji ambayo hajatibiwa ama kuchemshwa, kwa hivyo langu ni kuwahimiza wananchi wachukue tahadhari ya mapema hasa msimu huu wa mvua ili kuepuka magonjwa”, alisema Muthoni.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending