News
IEBC: Hatutaongeza muda wa usajili wa wapiga kura
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imesema haitaongeza mda wa usajili wa wapiga kura kote nchini.
Makamishna wa Tume hiyo wameshikilia kwamba wakati muda huo uliyotengwa utakapokamilika, basi itakuwa ndio mwisho wa zoezi hilo.
Tume hiyo ilisema japo tayari imesajili zaidi ya wakenya milioni moja licha ya kukadiria kusajili idadi ya wakenya milioni 6.5, juhudi hizo zimeonekana kutofikia malengo hitajika.
IEBC ilikuwa imetangaza kusajili wapiga kura wapya milioni 6.5 ikilenga vijana wa Gen Z katika zoezi hilo huku vijana wenyewe wakizindua mpango wa NIKO KADI kama mbinu mbadala ya kusajili idadi kubwa zaidi ya wapiga kura kote nchini, bado juhudi hizo zimeokena kutofikia malengo ya IEBC.
Kamishna wa IEBC Hassan Noor Hassan aliwarai vijana wa kizazi cha Gen Z kutopuuza zoezi hilo na kutumia muda uliyosalia wa kipindi cha wiki moja kujisajili kama wapiga kura, akisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha wakenya wanapata fursa ya kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu ujao.
Noor alisema vifaa vya usajili wa wapiga kura vya kieletroniki ama KIEMS KIT vimewasilishwa hadi mashinani na maafisa wa Tume hiyo wanafanya kila juhudi kuhakikisha wakenya wanaojitokeza kwa usajili huo wanasajili.
“Tumepeleka vifaa vya kusajili wapiga kura wapya hadi mashinani vya KIEMS KIT, na tuko na matumaini makubwa kwamba tutafikia idadi tunayolenga ya wapiga kura wapya milioni 6.5, na tunawarai wakenya kujitokeza kwa wingi na kujisajili kwa kutumia muda uliyosalia wa wiki moja”, alisema Noor.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

