Connect with us

News

Wapwani waonywa dhidi ya mafuriko

Published

on

Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini imetangaza kuendelea kushuhudiwa kwa vipindi vya mvua katika sehemu mbali mbali nchini kuanzia siku ya Jumatano Aprili 22 hadi tarehe 27 mwezi huu wa Aprili.

Idara hiyo ilitangaza kwamba viwango vya mvua vitaongezeka hadi milimita 20 katika muda wa saa 24 katika eneo la Pwani sawa na Kaskazini na Kusini Mashariki mwa nchi.

Miongoni mwa kaunti zitakazoathirika na mvua hizo ni pamoja na kaunti za Kwale, Mombasa, Taita-Taveta, Kilifi, Tana River, Lamu, Garissa na maeneo ya kaunti za Wajir, Mandera, Kitui na Makueni.

Idara hiyo imeonya wakaazi kusalia waangalifu hasa katika maeneo ambayo hukumbwa na mafuriko sawa na kutahadharisha kuhamia maeneo salama ili kuapuka majanga.

Katika taarifa iliyotumwa na idara hiyo kwa vyombo vya habari, ilisisitiza kwamba itakuwa ni hatua mwafaka iwapo wananchi watachukua tahadhari ya mapema na kujiepusha na mafuriko ambayo huenda yakashuhudiwa kutokana na mvua hizo.

Wakenya ambao wanaishi katika maeneo ya nyanda za chini wameshauriwa kuhamia maeneo salama ili kuepuka kusombwa na mafuriko ambayo mara nyingi husababishwa na mvua kubwa, huku ikizidi kuwarai wananchi kujiepusha kutembea maeneo ambayo yako na vidimbwi vya maji.

Idara hiyo pia iliwaonya madereva wa magari ya uchukuzi wa umma, kibinafsi na wale wa masafa marefu kuwa waangalifu wanapokuwa barabarani ili kuepuka utelezi wa magari ambapo mara nyingi husababisha ajali.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 umewasilishwa bungeni

Published

on

By

Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 na sheria za uchaguzi umewasilishwa katika bunge la Seneti.

Mswada huo unalenga kufanyia marekebisho kipengele cha Katiba cha 99 na 193 pamoja na sheria za uchaguzi sehemu ya 24 na 25 ili kuwepo na uwazi kwa magavana wanaolenga kuwania nyadhfa za uongozi baada ya kukamilisha mihula yao.

Mswada huo uliowasilishwa na Seneta wa Kirinyaga James Murango unalenga pia kuzuia magavana waliomaliza mihula yao ya uongozi kutowania nyadhfa za useneta, ubunge ama uwakilishi wadi, kwani inakuwa vingumu kuchunguzwa.

Kuwasilishwa kwa mswada huo bungeni kufuatia hali magavana kuwania wadhfa wa useneta baada ya kukamilisha mihula yao ya uongozi hali ambayo imeleta sintofahamu ya kiuongozi, ikiashiria tamaa za uongozi na njama ya kuhitilafiana na ufuatiliaji wa matumizi ya raslimali za umma.

Seneta Murango alisema katika utekelezaji wa majukumu yao, magavana hulazimika kuwajibika mbele ya mabunge ya kaunti na Seneti kuhusu matumizi ya kifedha na kiutawala.

Wakati huo huo alidokeza kwamba iwapo mswada huo utapishwa na kuwa sheria utasaidia kufutilia usimamizi wa raslimali za kaunti na matumizi ya fedha kwani utazuia magavana kuhitilafiana na uchunguzi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Serikali yaweka mikakati ya matumizi salama ya mtandao

Published

on

By

Serikali imeongeza juhudi za kuimarisha uaminifu, utawala bora na maendeleo ya kidijitali nchini, ikilenga kuhakikisha matumizi salama ya mtandao, yakuaminika na yanayowanufaisha wananchi wote.

Akizungumza jijini Mombasa wakati wa ufunguzi wa kongamano la chama cha ukaguzi na udhibiti wa mifumo ya habari, Waziri wa Habari na Uchumi wa Kidijitali William Kabogo alisema kuwa mabadiliko ya kidijitali nchini yameendelea kushika kasi kwa kiwango kikubwa.

Kabogo alisisitiza kuwa serikali imejizatiti kuweka mifumo madhubuti ya kulinda data na taarifa za watumiaji, huku pia ikihamasisha uwajibikaji katika matumizi ya teknolojia.

Kabogo aliongeza kuwa usalama wa mtandao ni nguzo muhimu katika kukuza uchumi wa kidijitali na kuvutia uwekezaji.

Taarifa ya mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending