Connect with us

News

Collins Hamis ahukumiwa kifungo cha miaka 31 gerezani

Published

on

Mahakama ya Kilifi imemhukumu kifungo cha miaka 31 gerezani Collins Hamis baada ya kupatikana na hatia ya kumnajisi mtoto mwenye umri wa miaka 16.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulusta baada ya ushahidi kuwasilishwa Mahakamani.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Obulutsa amesema hukumu hiyo itakuwa funzo kwa watu wenye tabia kama hizo katika jamii.

Awali upande wa mashtaka ulieleza Mahakama kwamba mnamo tarehe 16 mwezi Machi mwaka 2025 katika eneo la Chumani, eneo bunge la Kilifi kazkazini kaunti ya Kilifi, masaa ya usiku Collins alimvuta kwa nguvu mlalamishi akiwa ametoka Disco matanga na rafiki yake na kumsukuma hadi kwa kichaka alipokuwa amejificha na kuetekeleza kitendo hicho cha kimya cha kumnajisi na kumlawiti kisha kumtishia kumuua akiwa na panga.

Hakimu Obulutsa aidha alikemea vikali tabia za vijana wa bodaboda kuwadhulumu kingono watoto hususani katika sherehe za disco matanga, akiongeza kwamba suala la disco matanga limekuwa changamoto kubwa kaunti ya Kilifi hata baada ya serikali kupiga marufuku sherehe za disco matanga ambazo huchangia wasichana wadogo kudhulumiwa, bado zinaendelea kisiri.

Aidha Collins ameagizwa kuwa na siku 14 za kukata rufaa andapo hakuridhishwa na hukumu hiyo.

Taarifa ya Teclar Yeri.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi kutumia nguvu kukabiliana na wahalifu

Published

on

By

Huenda maafisa wa polisi wakutumia nguvu kupita kiasi katika kukabiliana na wahalifu ama wale wanaolenga kuzua vurugu na fujo mashinani.

Idara ya usalama nchini imesisitiza kwamba itakabiliana kikamilifu na magenge ya kihalifu ambayo yanaendeleza uhalifu mashinani na kutatiza shughuli za kibiashara, uchumi na usalama wa taifa.

Idara hiyo ilisema tayari imebaini magenge ya kihalifu ambayo yanatatiza usalama wa wananchi, huku wazazi wakilaumiwa kwa kuwatetea watoto wao licha ya kufahamu kwa tabia hiyo inazidi kuhatarisha maisha ya jamii mashinani.

Idara hiyo, ililalamikia kukithiri kwa utovu wa usalama hasa kaunti za Kwale, Mombasa na Lamu katika ukanda wa Pwani, kutokana na vijana wengi kuzama katika uraibu wa Mihadarati na ukosefu wa kazi, hatua iliyopelekea baadhi ya vijana kujiunga na magenge ya mapanga.

Kauli hiyo ya idara ya usalama ilijiri siku moja tu baada ya Kamanda wa Polisi kanda ya Pwani Ali Nuno, kuagiza maafisa wa polisi kuwapiga risasi magenge ya kihalifu ya vipanga kwa kutatiza usalama.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 umewasilishwa bungeni

Published

on

By

Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 na sheria za uchaguzi umewasilishwa katika bunge la Seneti.

Mswada huo unalenga kufanyia marekebisho kipengele cha Katiba cha 99 na 193 pamoja na sheria za uchaguzi sehemu ya 24 na 25 ili kuwepo na uwazi kwa magavana wanaolenga kuwania nyadhfa za uongozi baada ya kukamilisha mihula yao.

Mswada huo uliowasilishwa na Seneta wa Kirinyaga James Murango unalenga pia kuzuia magavana waliomaliza mihula yao ya uongozi kutowania nyadhfa za useneta, ubunge ama uwakilishi wadi, kwani inakuwa vingumu kuchunguzwa.

Kuwasilishwa kwa mswada huo bungeni kufuatia hali magavana kuwania wadhfa wa useneta baada ya kukamilisha mihula yao ya uongozi hali ambayo imeleta sintofahamu ya kiuongozi, ikiashiria tamaa za uongozi na njama ya kuhitilafiana na ufuatiliaji wa matumizi ya raslimali za umma.

Seneta Murango alisema katika utekelezaji wa majukumu yao, magavana hulazimika kuwajibika mbele ya mabunge ya kaunti na Seneti kuhusu matumizi ya kifedha na kiutawala.

Wakati huo huo alidokeza kwamba iwapo mswada huo utapishwa na kuwa sheria utasaidia kufutilia usimamizi wa raslimali za kaunti na matumizi ya fedha kwani utazuia magavana kuhitilafiana na uchunguzi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending