News
Collins Hamis ahukumiwa kifungo cha miaka 31 gerezani
Mahakama ya Kilifi imemhukumu kifungo cha miaka 31 gerezani Collins Hamis baada ya kupatikana na hatia ya kumnajisi mtoto mwenye umri wa miaka 16.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulusta baada ya ushahidi kuwasilishwa Mahakamani.
Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Obulutsa amesema hukumu hiyo itakuwa funzo kwa watu wenye tabia kama hizo katika jamii.
Awali upande wa mashtaka ulieleza Mahakama kwamba mnamo tarehe 16 mwezi Machi mwaka 2025 katika eneo la Chumani, eneo bunge la Kilifi kazkazini kaunti ya Kilifi, masaa ya usiku Collins alimvuta kwa nguvu mlalamishi akiwa ametoka Disco matanga na rafiki yake na kumsukuma hadi kwa kichaka alipokuwa amejificha na kuetekeleza kitendo hicho cha kimya cha kumnajisi na kumlawiti kisha kumtishia kumuua akiwa na panga.
Hakimu Obulutsa aidha alikemea vikali tabia za vijana wa bodaboda kuwadhulumu kingono watoto hususani katika sherehe za disco matanga, akiongeza kwamba suala la disco matanga limekuwa changamoto kubwa kaunti ya Kilifi hata baada ya serikali kupiga marufuku sherehe za disco matanga ambazo huchangia wasichana wadogo kudhulumiwa, bado zinaendelea kisiri.
Aidha Collins ameagizwa kuwa na siku 14 za kukata rufaa andapo hakuridhishwa na hukumu hiyo.
Taarifa ya Teclar Yeri.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

