Connect with us

News

Wapwani waonywa dhidi ya mafuriko

Published

on

Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini imetangaza kuendelea kushuhudiwa kwa vipindi vya mvua katika sehemu mbali mbali nchini kuanzia siku ya Jumatano Aprili 22 hadi tarehe 27 mwezi huu wa Aprili.

Idara hiyo ilitangaza kwamba viwango vya mvua vitaongezeka hadi milimita 20 katika muda wa saa 24 katika eneo la Pwani sawa na Kaskazini na Kusini Mashariki mwa nchi.

Miongoni mwa kaunti zitakazoathirika na mvua hizo ni pamoja na kaunti za Kwale, Mombasa, Taita-Taveta, Kilifi, Tana River, Lamu, Garissa na maeneo ya kaunti za Wajir, Mandera, Kitui na Makueni.

Idara hiyo imeonya wakaazi kusalia waangalifu hasa katika maeneo ambayo hukumbwa na mafuriko sawa na kutahadharisha kuhamia maeneo salama ili kuapuka majanga.

Katika taarifa iliyotumwa na idara hiyo kwa vyombo vya habari, ilisisitiza kwamba itakuwa ni hatua mwafaka iwapo wananchi watachukua tahadhari ya mapema na kujiepusha na mafuriko ambayo huenda yakashuhudiwa kutokana na mvua hizo.

Wakenya ambao wanaishi katika maeneo ya nyanda za chini wameshauriwa kuhamia maeneo salama ili kuepuka kusombwa na mafuriko ambayo mara nyingi husababishwa na mvua kubwa, huku ikizidi kuwarai wananchi kujiepusha kutembea maeneo ambayo yako na vidimbwi vya maji.

Idara hiyo pia iliwaonya madereva wa magari ya uchukuzi wa umma, kibinafsi na wale wa masafa marefu kuwa waangalifu wanapokuwa barabarani ili kuepuka utelezi wa magari ambapo mara nyingi husababisha ajali.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending