Connect with us

News

Shule Ya Upili Ya Serani Ndiyo Mabingwa Eneo La Mvita

Published

on

Timu ya shule ya upili ya Serani imetetea ubingwa wao wa eneo la Mvita baada ya kuwalaza Tononoka magoli 2-1 katika fainali iliyochezewa kwenye uwanja wa shule ya upili ya Khamis.

Emanuel Oroni aliwatanguliza Serani na goli la kwanza kupitia mkwaju wa penati kabla ya Ali Abdallah kusawazishia Tononoka, lakini goli lake Emanuel Ngala katika kipindi cha pili likawapa ubingwa huo.

Kulingana na kocha wa Serani Alex Shikanga ni kwamba wamekua na mazoezi kambambe kabila ya mashindano ya shule za Upili na walikua wanasubiri ushindi tu wala si kitu kingine.

“Tulikua tumejiandaa kwa ajili ya ushindi pekee tumekua na maandalizi mazuri na hivyo nilijua tuatshinda fainali hii,katika miaka mitano tumepoteza taji hili mara moja pekee.”

kwa upande wake kocha wa Shule ya Upili ya Tononoka Juma ALi Kalato amesema kwamba amesema kwamba amekubali matokeo baada ya changamoto si haba kabila ya mechi hiyo ya fainali baadhi ya wachezaji wakingonjeka.

“Nashukuru Mwenyemezi Mungu tumefika fainali na vijana wangu wamepambana kiume kwani kabila ya mechi tulikua na wagonjwa ila wamepambana inshallah tutashinda uko mbele.”

Katika upande wa wasichana Kaa Chonjo wameibuka mabingwa kwa kuwalaza Mekatitilili magoli 3-0.

Serani na  Tononoka wataiwakilisha Mvita katika ngazi ya kaunti upande wa wavulana, na Kaa Chonjo na Mekatililii wakiwakilishja upande wa wasichana.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending