News
Ujenzi wa daraja la Mwachande latoa matumaini ya miaka kwa wakaazi
Kwa miaka mingi, wakaazi wanaotumia kivuka cha Mto Ramisi eneo la Mwachande kaunti ya Kwale, wamekabiliwa na changamoto wanapotafuta njia za kufuka daraja hilo dogo linalounganisha Msambweni na Lunga Lunga.
Wakati wa msimu wa mvua, wakaazi wanasema kivuko cha zamani ilikuwa vigumu zaidi kutumia na wakati mwingine kuwa hatari jambo lililokatiza safari za kwenda sokoni, shuleni, vituo vya afya na maeneo ya kazi.
Ujenzi wa Daraja la Mwachande umebadilisha hali hiyo na kuleta matumaini ya usafiri salama pamoja na kuimarika kwa shughuli za kiuchumi katika eneo hilo.
Daraja hilo linalojengwa na Mamlaka ya Barabara za mitaa (KeRRA) pamoja na barabara ya Milalani–Kikoneni–Mwangulu, kwa gharama inayokadiriwa kuwa shilingi milioni 538 inalenga kusahisisha shughuli za usafriki.
Kulingana na Mwanamisi Mwaruma, umuhimu wa mradi huu haupimwi kwa saruji na maelezo ya uhandisi, bali kwa kuhakikisha usafiri rahisi, akisema wakaazi wamevumilia miaka mingi na changamoto nyingi lakini ujenzi wa daraja hilo utarahisha shughuli za uchukuzi.
“Kwetu, tofauti kubwa zaidi ni kwamba usafiri utakuwa rahisi sasa. Tumeteseka hapa kwa miaka mingi, hasa wakati wa mvua,” alisema Mwaruma.

Wakaazi wa Mwachenda wapongeza ujenzi wa daraja la Mwachenda katika mtu Ramisi
Kwa upande wake mkaazi wa eneo hilo Suleiman Muhammed, alisema maendeleo ya mradi huo yanawakilisha kutimizwa kwa ombi la muda mrefu la jamii.
“Tumelisubiri daraja hili kwa muda mrefu sana. Kinachotuhusu ni kuona kazi hatimaye ikiendelea na kujua kwamba watu wataweza kuvuka kwa usalama,” aalisema Suleiman.
Baadhi ya wakaazi waliepongeza utawala wa Rais William Ruto kwa kusukuma mradi huo kuelekea kukamilika, wakisema wanatumaini kuwa muunganiko huo ulioboreshwa utaongeza biashara, kupunguza changamoto za usafiri na kurahisisha familia kufikia huduma muhimu.
Kwa wakazi wa Mwachande, manufaa hayo yanatarajiwa kuwa ya moja kwa moja — vivuko salama zaidi, safari fupi, urahisi wa kusafirisha mazao ya kilimo, upatikanaji bora wa masoko na kupungua kwa usumbufu wakati wa mvua kubwa.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Wakaazi wa Voi wapendekeza mbinu mpya za kulipa ada za maji
Wakaazi wa kaunti ndogo ya Voi kaunti ya Taita Taveta wanapendekeza kampuni ya kusambaza maji mjini humo ya TAVEVO kubuni mbinu mpya ya kulipia ada ya maji kama ile ya kulipia umeme (Token) ili kumwezesha mteja wa maji kulipia kwa gharama anayoimudu.
Kulingana na wakaazi wengi wao wanakosa bidhaa hiyo muhimi ya maji kutokana na gharama ya juu wanayotozwa.
Walisema ikiwa kampuni hiyo ya kusambaza maji itakubali mapendekezo hayo huenda ikawapunguzia gharama ya kulipia maji.
‘’Kama tunaweza kuletewa Token wengi wetu tutaweza kulipa kwa gharama tunayoweza kumudu kuliko ile mita isome mpaka mwezi.Wengine wanashindiwa katikati wanakatiwa’’ alisema mkaazi
Wakati huo huo, wakaazi hao pia walishinikiza kampuni hiyo ya kusambaza maji ya Tavevo kubadilisha mita za zamani za maji na kuweka za plastic kama njia mojawapo ya kukabiliana na wizi wa mita hizo ambazo huwa zinang’olewa na kuuzwa kwa wanaonunua vyuma kuukuu.
‘’Sahizi tumekuwa na shida ya hizi mita, mita zang’olewa na sasa mimi nilikuwa napendekeza kama zinawezwa kubadilishwa na kuwekwe za plastiki kwa sababu inasemekana zinaibwa ziende ziuzwe kwa watu wa kununu scrap’’ aliongeza mkaazi.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Vita dhidi ya dhulma za kijinsia vyaendelezwa Kilifi
Visa vya ukatili wa kijinsia (GBV), dhidi ya wanawake na watoto katika kaunti ya Kilifi vinapoendelea kushuhudiwa, mikakati ingali inaendelezwa katika kuhakikisha vinadhibiti vilivyo.
Akizungumza baada ya kuzindua mchakato wa kuhamasisha jamii kuhusu visa hivyo, mwanaharakati na pia mwanzilishi wa shirika la Dada Yangu, Fatuma Ramadhan alisema kwa ushirikiamo na wadau mbalimbali wanalenga kuhakikisha jamii inapata elimu ya namna ya kukabiliana na ukatili huo wa kijinsia.
Fatuma Ramadhan pia alisema wanawake ndio waathiriwa wakuu wa dhuluma za kijinsia kupitia mitandao.
‘’Visa hivi vimekuwa vingi na ndio maana kuna haja ya kila mmoja kushiriki ipasavyo Katika kuhakikisha visa hivi vinadhibitiwa vilivyo na sio kuachia mashirika ya kijamii pekee’’ Alisema Ramadhan
Kwa upande wake Michael Baraka ambaye ni mhudumu wa bodaboda alisema watashirikiana katika kuripoti matukio hayo ili kudhibiti visa hivyo na kuitaka jamii kuondoa dhana kuwa vijana wa bodaboda wanahusika pakubwa katika utekelezaji wa dhuluma hizo.
‘’Kama wahudumu wa bodaboda tutashirikiana na kila mmoja kufanikisha hilo na pia kwa niaba ya wenzangu ningependa jamii iondoe dhana kuwa sisi tunahusika pakubwa katika visa vibaya’’ alisema Baraka.
Naye Shyleen Mumanyi wa shirika la Young Women Leadership Institute alisema katika kuhakikisha visa hivyo vinadhibitiwi watashirikiana pia na machifu na wazee wa nyumba kumi miongoni mwa viongozi wingine katika jamii.
Ni kauli ambayo iliungwa mkono na Abdulfah Nurein Mohamed huku akisema visa hivyo hasa kwa watoto huwa vinaongezeka zaidi wakati shule zimefungwa na kutoa wito kwa serikali ya kaunti ya Kilifi kuweka mikakati ifaayo katika kuimarisha usalama hasa katika fuo za habari na kusisitiza umuhimu wa wazee wa mtaa kujukumika vilivyo katika utendakazi wao.
Kwa kauli moja walikemea visa vya ukatili wa kijinsia pamoja na vile vya watu kupotea katika hali tatanishi na kutoa wito kwa serikali kuu kufanya uchunguzi wa visa hivyo kwa wakati na watuhumiwa wakabiliwe kisheria na pia kufanya kazi kwa karibu na mashirika yayototetea haki za wanawake.
Taarifa ya Janet Mumbi

