Connect with us

News

Vifo vya Wanawake wajawazito Kilifi

Published

on

Kaunti ya ni Kilifi ni miongoni mwa kaunti ambazo ziko na Idadi kubwa ya vifo vya wanawake wajawazito wanaofariki dunia wakati wa kujifungua pamoja na vile vya watoto wachanga.

Katika kikao ambacho kiliwaleta pamoja waandishi wa habari, hafla ambayo ilfanyika katika ukumbi wa kibaoni mjini Kilifi, kupitia wakfu wa Shina ilibainika visa hivyo vinachangiwa na ukosefu wa hamasa kwa akina mama wajawazito hasa walioko mashinani kuhusu umuhimu wa kula lishe bora, kutokuhudhuria kliniki kutokana na mila na tamaduni na pia hali ya umasikini.

Akizungumzia hilo Nazi Kivutha ambaye ni mwanzilishi wa wakfu wa Shina alisema kando na ukosefu wa ufahamu huo wa akina mama kuhusu uzazi usalama kaunti ya Kilifi hamasa za kutosha hazijatolewa ipasavyo maeneo ya mashinani.

“Hapa kaunti ya Kilifi viwango vya umasikini viko juu na hilo linawafanya wanawake wengi kushindwa kumudu lishe bora na pia wengi wao bado wamekumbatia mila na tamaduni na ndio maana wanaamini kukandwa na wakunga na kupuuza kuhudhuria kliniki ili kujifungua Salama” alisema Bi Kivutha

Kwa upande wake Winnie Barawa alisema baadhi ya wanawake wajawazito wanafariki dunia kutokana ukosefu wa damu mwilini hali ambayo inachangia kwa vifo hivyo na kuwataka kuzingatia ulaji wa vyakula bora na pia kuhudhurikia kliniki mara kwa mara.

“Utapata wengi kiwango chao damu kiko chini mno hali ambayo inawaweka  mama na mtoto katika hatari ya kufariki dunia” alisema Winnie Barawa.

Hata hivyo walisema kupitia mradi wa okoa mama na mtoto chini ya wakfu wa Shina mikakati inaendelea kuwekwa ili kudhibiti vifo hivyo.

Haya yanajiri miezi michache baada ya mratibu wa huduma ya afya kaunti ya Kilifi Edward Mumbo kutoa takwimu hizo zikiwemo zile za  watoto njiti

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakimbizi nusu milioni wakabiliwa na baa la njaa, Dadaab

Published

on

Ripoti iliyotolewa hivi karibu na Shirika la Chakula duniani WFP ilionyesha kwamba zaidi ya wakimbizi nusu milioni wanaoishi katika kambi za wakimbizi za Kakuma na Dadaab zilizoko nchini Kenya, wako katika hatari ya kuangamia kutokana na baa la njaa.

Kambi hizi ambazo zinahifadhi wakimbizi wengi zaidi kutoka nchini Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Somalia, ziko hatari iwapo zitakosa misaada ya chakula.

Kufuatia hali hiyo ambayo pia imechangiwa na mashirika ya kimataifa kusitisha ufadhili, sasa hali huenda ikawa tofauti baada ya taifa la Korea kwa ushirikiano na Kenya kutoa ufadhili wa shehena ya nafaka ya zaidi ya tani elfu 10 ambayo inakadiriwa kuwa kima cha shilingi milioni 1.2.

Katibu katika Idara ya uhamiaji nchini Belio Kipsang, aliyepokea msaada huo wa Chakula mjini Mombasa na kuhifadhiwa katika maghala ya Shirika la WFP, ameonya kwamba iwapo Kenya itakosa kupokea msaada kutoka kwa washirika na wafadhili wengine, basi italazimika kuchukua maamuzi magumu, ikiwemo kuwaondoa baadhi ya wakimbizi.

“Nyuma ya kila takwimu kuna familia ambazo ustahimilivu wao unaendelea kujaribiwa kila siku: akina mama wanaokosa kula ili watoto wao wapate chakula, watu walio katika mazingira hatarishi wakiruka milo, na vijana wanaokabiliwa na mustakabali usio na uhakika. Hizi si takwimu za kufikirika. Zinawakilisha watu halisi ambao heshima yao, afya yao na matarajio yao ya maisha yanategemea maamuzi tunayofanya kwa pamoja,” alisema.

Wakati wa hafla hiyo ya kupokea msaada huo wa chakula kwa wakimbizi wa Kakuma na Dadaab, Mkurugenzi wa Shirika la WFP nchini Kenya Betty Ka, alisema shehena ya nafaka itasaidia kuwahudumia takribani wakimbizi nusu milioni katika miezi ijayo.

“Usafirishaji huu unaonyesha umuhimu wa ushirikiano imara katika mnyororo wa ugavi wa misaada ya kibinadamu, ambapo ushirikiano huu kati ya Kenya, Mamlaka ya bandari Kenya (KPA), Shirika la viwango la Kenya(KEBS) na mpango wa Chakula Duniani (WFP) kwa kuhakikisha kwamba chakula cha msaada kinafanikishwa”,alisema Betty.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

NCTC yaanzisha hamasa mashinani kudhibiti ugaidi

Published

on

By

Kituo cha kitaifa cha kukabiliana na ugaidi yaani National Counter Terrorism Centre (NCTC) kimeanzisha mpango wa kutoa hamasa za kuwaepusha wananchi na masuala ya ugaidi hasa maeneo ya Shakahola katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Akizungumza katika eneo hilo, Afisa mkuu wa kituo hicho Grace Kaparo aliwataka wazazi kufuatilia kwa ukaribu mienendo ya watoto wao kama njia mojawapo ya kuzuia michipuko ya makundi ya ugaidi.

Kaparo alidokeza kwamba mpango huo unalenga kupunguza visa vya uhalifu miongoni mwa vijana sambamba na kuwajengea mustakabali bora wa maisha yao.

Hamasa hiyo inajiri baada ya kushughudiwa maafa ya watu zaidi ya 400 katika msitu wa Shakahola kutokana na mafunzo ya itikadi kali huku mshukiwa mkuu wa mauaji hayo akiwa katika mikono ya maafisa wa polisi.

“Tumekuja Shakahola kuelimisha jamii kuepusha makundi ya kigaidi na jinsi ya kutambua watu walio na itikadi kali ili kuepusha watu kuangamia kama hapa Shakahola watu wangekuwa na ufahamu wangeepuka maafa”, alisema Grace.

Kwa upande wake Naibu Kamishna eneo Malindi kaunti ya Kilifi Harrison Matevwa aliwataka maafisa wa utawala eneo hilo kuendeleza hamasa za mara kwa mara kwa wakaazi wa maeneo yao ili kutathmini changamoto zinazowakumba na kuzitatua mara moja.

“Naiambia kamati ya usalama eneo hili kutembea na kufanya baraza za usalama kuweza kuskia ile wananchi wanapitia kwa sababu wengi wanakosa usaidizi ndio watu wahalifu wakija wanaweza kuwapotosha”alisema Harrison.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending