Connect with us

News

Wakaazi Kilifi washinikiza serikali kukusanya maoni kabla miradi kuanza.

Published

on

Serikali kuu imeandaa kikao cha kukusanya maoni ya umma pamoja na wadau mbali mbali kuhusu miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya kitaifa kaunti ya Kilifi katika chuo kikuu cha pwani.

Akizungumza katika kikao hicho katibu mkuu wa maswala ya uratibu katika ofisi ya mkuu wa mawaziri Ahmed Abdisalam, alisema kikao hicho kinatoa fursa kwa wananchi kufahamu namna serikali inavyotekeleza miradi yake kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Abdisalam aliongeza kuwa wananchi wanamchango mkubwa katika kutambua changamoto zozote zinazojitokeza kwenye mchakato wa utekelezaji wa miradi hiyo, akidokeza kuwa kaunti ya kilifi ni miongoni mwa kaunti zinazofaidi miradi mingi ya serikali.

“Tunataka kuhakikisha tunatembea na wananchi kutoka hatua ya kutambua miradi, utekelezaji na pia inapokamilika, malengo ni kusistiza uhusika wa wananchi ili kuwa na uendelevu wakati wa kutekeleza miradi ya serikali kuu”, alisema Abdisalam.

Kwa upande wake kamishna wa kaunti ya Kilifi Josephat Biwot alidokeza kuwa serikali kwa sasa inaendeleza miradi mbali ikiwepo ujenzi wa nyumba za bei nafuu eneo la Tezo na Mtwapa pamoja na ujenzi wa soko eneo la Watamu.

Biwot vile vile alisema serikali inajenga vyumba vya malazi ya zaidi ya wanafunzi 1,700 katika chuo kikuu cha pwani pamoja na ujenzi wa barabara ya Bamba kuelekea Ganze huku ile ya Mwakirunge ikitarajiwa kuanza karibuni.

“Tuko na miradi mipya iliyoanzishwa na serikali iliyomamlakani kama ujenzi ya nyumba za bei nafuu, tuko na miradi wa Tezo na Mtwapa ambayo inaendelea na pia tuko na ujenzi wa masoko unaendelea, watamu liko zaidi ya asilimia 70 kukamilika”, alisema kamishna Biwot.

Kwa upande wao baadhi ya wanachi waliohudhuria kikao hicho waliikata serikali kuhakikisha inahusisha wananchi kabla miradi kuanza kutekelezwa, wakidai serikali imekuwa ikitafuta maoni ya umma wakati miradi ikiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending