News
Wakaazi wa maeneo kame wahakikishiwa usalama wa chakula
Serikali imehakikishia wakaazi wa kaunti 23 nchini ambazo zinakabiliwa na makali ya ukame kwamba inachakula cha kutosha cha kuwawezesha kukabiliana na makali ya njaa.
Akizungumza katika kaunti ya Tanariver baada ya kuongoza ugawaji chakula kwa waathiriwa, waziri wa utumishi wa umma Geoffrey Ruku, alisema hakuna mkenya atakayeaga dunia kwa kukosa chakula.
Waziri Ruku alisema msaada wa chakula hicho ni kwa ajili ya familia zisizo na uwezo katika jamii huku akiwataka maafisa wa utawala wa mkoa kutoa ripoti kuhusu walagahai wa chakula cha msaada.
Wakaazi wa maeneo ya Tanariver wameitaka serikali kubuni mikakati ya Kukabiliana na athari za kiangazi vile vile mafuriko.
Wakati huo huo mbunge wa Garsen katika kaunti ya Tanariver Ali Wario alishinikiza serikali kuu kuongeza mgao wa chakula kwa familia zinazoishi maeneo yanayokabiliwa na makali ya njaa.
Wario alisema msimu wa mwezi mtukufu wa Ramadhan unakaribia na familia zilizoathirika na ukame na mafuriko zinafaa kuzingatiwa hata na zaidi upande wa msaada wa chakula.
Wario alibainisha kuwa usalama wa chakula unafaa kupewa kipaumbele hasa kwa jamii maskini ili kuepusha mahangaiko na maafa.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

