Connect with us

News

Wakaazi wa maeneo kame wahakikishiwa usalama wa chakula

Published

on

Serikali imehakikishia wakaazi wa kaunti 23 nchini ambazo zinakabiliwa na makali ya ukame kwamba inachakula cha kutosha cha kuwawezesha kukabiliana na makali ya njaa.

Akizungumza katika kaunti ya Tanariver baada ya kuongoza ugawaji chakula kwa waathiriwa, waziri wa utumishi wa umma Geoffrey Ruku, alisema hakuna mkenya atakayeaga dunia kwa kukosa chakula.

Waziri Ruku alisema msaada wa chakula hicho ni kwa ajili ya familia zisizo na uwezo katika jamii huku akiwataka maafisa wa utawala wa mkoa kutoa ripoti kuhusu walagahai wa chakula cha msaada.

Wakaazi wa maeneo ya Tanariver wameitaka serikali kubuni mikakati ya Kukabiliana na athari za kiangazi vile vile mafuriko.

Wakati huo huo mbunge wa Garsen katika kaunti ya Tanariver Ali Wario alishinikiza serikali kuu kuongeza mgao wa chakula kwa familia zinazoishi maeneo yanayokabiliwa na makali ya njaa.

Wario alisema msimu wa mwezi mtukufu wa Ramadhan unakaribia na familia zilizoathirika na ukame na mafuriko zinafaa kuzingatiwa hata na zaidi upande wa msaada wa chakula.

Wario alibainisha kuwa usalama wa chakula unafaa kupewa kipaumbele hasa kwa jamii maskini ili kuepusha mahangaiko na maafa.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya iliyotoa kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

Trending