News
Wito wa haki kupatikana watawala mazishi ya Albert Ojwang’
Ibada ya mazishi kwa ajili ya mwendazake mwanablogu na mwalimu Albert Ojwang’ aliyeuawa mikononi mwa polisi inafanyika katika shule ya msingi ya Nyawango kaunti ya Homa Bay, huku kukiwa na hali ya taharuki.
Katika hafla hiyo uwepo wa maafisa wa usalama haujashuhudiwa.
Kulingana na Odhiambo Ojiro, mmoja wa wanaharakati katika eneo hilo alisema vijana wamejitolea kumpumzisha Ojwang’ kwa heshima aliyostahili’ na ishara hiyo imeonyesha umoja walionao vijana hao.
Wakizungumza katika hafla hiyo, baadhi ya walimu katika shule ambayo Albert alikuwa akihudumu katika kaunti ya Taita Taveta, wakiongozwa na Ismael Omoke Kongo walishinikiza naibu inspekta jenerali wa Eliud Lagat na wengine waliohusika na mauaji hayo kukamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani.
Walisema kesi ya mauaji ya dhidi ya Albert inafaa kuchukuliwa kwa uzito na kuharakishwa mahakamani ili haki kwa familia na jamii ipatikane.
“Tunataka hii kesi kuharakishwa na wote waliohusishwa iwe kupitia kutoa maagizo hadi utekelezaji kushtakiwa”, walisema walimu hao
Wanablogu mbali mbali waliofika katika hafla hiyo waliunga mkono kauli ya walimu hao huku wakishikiniza mamlaka ya kutathmini utendakazi wa polisi IPOA na idara ya upelelezi wa makosa ya jinai DCI kuwajibika.
“Yale ambayo mnatenda Mungu anaona, ipo siku sauti zetu zitasikika, mimi naambia IPOA na DCI mnatatiza haki kwa Albert na nataka mmkamate mshtakiwa, na tunaambia serikali huwezi kutuua na utuongoze”, walisema wanablogu.
Ojwang’ alichukuliwa nyumbani kwao kaunti ya Homabay na maafisa wa usalama na kusafirishwa hadi kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi ambapo alitangazwa kufariki baadaye.
Wakati huo polisi walitoa taarifa na kudai Albert alifariki baada ya kujigonga kwenye ukuta wa chumba cha seli alimokuwa anazuiliwa kituoni Central.
Mauaji ya Albert yalizua hasira miongoni mwa wakenya hasa vijana wa kizazi cha Gen Z, ambao wamekuwa wakiendeleza misururu ya maandamano nchini.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali
Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.
Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.
Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.
Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.
Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.
Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.
Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.
Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.
Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa
Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.
Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.
Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.
“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

