News
Beacco: Serikali itahakikisha wafungwa wanawezeshwa ili kusaidia jamii zao
Katibu katika Idara ya huduma za magereza nchini Dkt. Salome Beacco amesema serikali itahakikisha wafungwa wanapata mazingira bora ya afya, elimu na jamii ili kuwawezesha kurejea katika jamii wakiwa watu waliobadilika.
Dkt. Beacco alisema serikali inaendeleza mpango wa kuboresha magereza nchini, ikiwemo kutoa vitanda vipya, mavazi, huduma za maji safi na mafunzo ya stadi za maisha kwa wafungwa pamoja na kushughulikia maslahi ya maafisa wa magereza.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maktaba iliyoboreshwa katika gereza la Jela baridi eneo la Mvita kaunti ya Mombasa, Dkt. Beacco alisema mradi huo ulifadhiliwa na jamii ya Dawoodi Bohras, utachangia kuwapa wafungwa matumaini na dira mpya maishani.
“Tuko na mipango bora kama serikali kuhakikisha wafungwa wanawezeshwa na kuwa katika mazingira bora ya afya, elimu na jamii ili kuwawezeshwa kurejea katika jamii wakiwa watu waliobadilika”, alisema Beacco.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirika linaloshughulikia waraibu na wagonjwa wa afya ya akili, Amina Abdallah alieleza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika kuendeleza miradi ya maendeleo kwenye magereza.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

