Connect with us

National News

Ufisadi Humu Nchini Umekuwa Tatizo, Koome Asema

Published

on

Photo: Courtesy

Jaji mkuu nchini Martha Koome ameelezea kutamaushwa na ufisadi ambao bado umekithiri katika idara mbalimbali za umma, akisema ufisadi humu nchini umekuwa tatizo la kitaifa ambalo limeathiri maendeleo.

Akizungumza jmjini Mombasa wakati wa kongamano la baraza la kitaifa kuhusu utawala na haki, Jaji Koome amesema idara za haki zina jukumu kubwa la kuzuia, kuchunguza, kulinda, kusikiliza na kutoa hukumu katika kesi za ufisadi.

Jaji Koome, amesema idara ya Mahakama nchini imeanzisha mchakato wa kubuni sera za kupambana na ufisadi zitakazokamilika na kuzinduliwa rasmi mwezi Machi mwaka huu, na kwamba mapambano dhidi ya rushwa na uhalifu wa kiuchumi ni jukumu la kila mmoja.

Wakati uo huo amesema wataimarisha ushirikiano, uwezo, kuboresha mfumo wa kisheria, sera na utawala, kuimarisha ufanisi na uwajibikaji katika vita dhidi ya ufisadi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Umoja wa mataifa wapunguza bajeti yake kwa bola milioni 577

Published

on

By

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amependekeza kupunguzwa kwa bajeti ya umoja huo ya mwaka ujao kwa dola milioni 577, hatua ambayo itapunguza asilimia 18 ya kazi.

Akizungumza mbele ya kamati ya bajeti ya Baraza kuu la umoja wa mataifa, Guterres alisema umoja huo bado haujapokea mchango wa karibu dola milioni 900 kutoka kwa wanachama mwaka huu wa 2025.

Umoja wa mataifa unapendekeza bajeti ya dola bilioni 3 kwa mwaka 2026, ikiwa na upungufu wa asilimia 15 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka huu.

Umoja wa Mataifa unakabiliwa na mgogoro wa kifedha uliosababishwa pakubwa na hatua ya Marekani kutolipa ada yake, kutokana na sera mpya za Rais Donald Trump.

Hatua hii ya umoja wa mataifa huenda ukachangia changamoto kubwa kwa mataifa wanachama hasa yanayotegemea pakubwa juhudi za umoja huo katika masuala mbalimbali ikiwemo usalama.

Continue Reading

Editor's Picks

Bangi Yanaswa Daraja la Sabaki – Malindi, Kaunti ya Kilifi

Published

on

Maafisa wa Usalama wamenasa shehena ya Bangi katika daraja la Sabaki, Mjini Malindi Kaunti ya Kilifi, iliyokuwa imefichwa kwenye makasha ndani ya basi lililokuwa likisafiri kitoka Lamu kwenda Mombasa.

Basi hilo lilisimamishwa na Maafisa wa usalama katika kizuizi Cha Polisi kilichoko daraja hilo kwa shughuli ya kawaida ya ukaguzi wa magari na mizigo, ambapo magunia mawili ya bangi hiyo yalipatikana yamefichwa katika sehemu ya Mizigo ndani ya basi hilo.

Dereva na Kondakta wa basi hilo, mali ya kampuni ya mabasi ya Tawakal, walikamatwa, ingawa abiria anayeaminika ndiye mwenye kusafirisha bangi hiyo alitotoka mtego huo na bado anatafutwa na Maafisa Polisi.

Waliokamatwa sasa wanazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Mjini Malindi huku uchunguzi zaidi unapoendelea.

Maafisa hao wanasema, walipata vidokezo kuhusiana na bangi hiyo ambayo bado haijajulikana thamani yake.

Katika siku za hivi karibuni, Daraja hilo la Sabaki limekuwa chini ya oparesheni kali ya maafisa wa usalama kutokana kuongezeka Kwa idadi ya vyombo vya usafiri, hasa Malori ambayo yaaminika kutumika kwa zaidi kwa biashara haramu kutoka Kaunti za Tana River na Lamu kuingia Kaunti za Kilifi na Mombasa.

Dereva huyo na Kondakta wake watafikishwa mahakamani hivi karibuni huku maafisa wa Polisi wakitia wito kwa wanachi kutoa habari zitakazosaidia kumtia nguvuni mshukiwa mkuu.

Continue Reading

Trending