Connect with us

News

Bilioni 2.3 kuisaidia kupiga vita dhuluma za kijinsia kaunti ya Kilifi

Published

on

Kaunti ya Kilifi ni moja wapo ya kaunti 47 zinazokabiliwa na changamoto za dhulma za kijinsia, mimba za utotoni, umaskini, mila na tamaduni potovu na mifumo duni ya afya ya jamii.

Takwimu za hivi punde, zinatoa picha ya wasiwasi kwani kufikia Oktoba mwaka wa 2024, zaidi ya wasichana 7,000 katika kaunti ya Kilifi walikuwa wamejifungua wakiwa na umri mdogo.

Ingawa idadi hiyo ilipungua hadi takriban 4,500 mwaka huu, idadi hiyo inasalia kuwa kubwa mno na kuwafanya viongozi wa eneo hilo na watetezi wa watoto kutoa wito wa kuwepo kwa juhudi za haraka za kulinda wasichana wadogo na kutafuta suluhisio la kudumu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango wa STRIDES for SRHR through Resilient Health Systems (STRIDES) katika kituo cha Afya cha Ganze, kaunti ya Kilifi, Naibu Gavana wa Kilifi Flora Mbetsa Chibule alitaja hali hiyo kuwa ya kusikitisha sana.

“Kilifi, ni kati ya kaunti nyingi katika taifa letu, inaendelea kukabiliwa na changamoto za kipekee katika kuhakikisha kila kijana na kila mwanamke anafurahia haki ya kupata huduma bora za afya,” alisema Flora.

Mpango wa STRIDES for SRHR through Resilient Health Systems (STRIDES) katika kituo cha Afya cha Ganze

Aidha alielezea wasiwasi wake juu ya kuongezeka kwa visa vya unajisi na kujamiiana na watu wa ukoo, akiwaonya wahalifu wanaowadhulumu wasichana walio katika mazingira magumu, hasa kutoka kwa familia zenye umaskini.

Kulingana na Mkurugenzi Mtendaji wa Wakfu wa Aga Khan Kenya, Susan Otieno, mradi wa STRIDES ni ushirikiano wa miaka saba (2025–2032) wenye thamani ya takriban shilingi bilioni 2.3, unaofadhiliwa na Serikali ya Canada, zitasaidia pakubwa kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia kaunti ya Kilifi.

Mpango huo utatekelezwa kupitia muungano wa washirika ikiwemo Chuo Kikuu cha Aga Khan (AKU), huduma za afya za Aga Khan (AKHS), Kituo cha kimataifa cha afya ya uzazi Kenya (ICRHK), na Moving the Goalposts (MTG)—kwa ushirikiano na Serikali ya kaunti ya Kilifi.

Mpango huo utalenga kaunti ndogo tano—Kilifi Kaskazini, Kaloleni, Rabai, Malindi, na Ganze kwa lengo la kupunguza mimba za utotoni, kupambana na dhulma za kijinsia na kuimarisha uhusiano kati ya jamii na vituo vya afya.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending