Connect with us

News

Chuo cha kiufundi cha Godoma taabani

Published

on

Ripoti iliyotolewa na Wizara ya elimu nchini kuhusu vyuo vya kiufundi vya TVETs ilibaini kwamba idadi ya wanafunzi wanaojiunga na vyuo hivyo bado iko chini mno.

Hii ni baada ya vijana wanaofaa kujiunga na vyuo hivyo kusalia nyumbani licha ya serikali kutumia raslimali za umma kujenga taasisi hizo muhimu hadi mashinani.

Chuo cha kiufundi cha Godoma kilichoko eneo la Vitengeni katika eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi huenda kikawa kati ya vyuo vitakavyofungwa kutokana na idadi ndogo ya wanafunzi.

Kati ya wanafunzi 500 katika chuo hicho, asilimia 80 ya wanafunzi hao ni wale waliotumwa na Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS huku asilimia 20 wakiwa wanafunzi kutoka eneo bunge la Ganze na sehemu zengine za nchi, hali inayoibua wasiwasi.

Hatua hii iliwalazimu wadau wa sekta ya elimu kutoka serikali kuu, maafisa wa usalama, wakaazi pamoja na machifu kwa ushirikiano na usimamizi wa chuo hicho kufanya mkutano wa kuangazia jinsi watakavyosajili wanafunzi.

Katika mkutano uliyoandaliwa katika chuo hicho cha kiufundi cha Godoma, ulibaini sababu zilizochangia wanafunzi kuondoka chuoni na wengine kusalia nyumbani, mojawapo ikiwa ongezeko la karo kinyume na taasisi zengine.

Chuo hicho ambacho awali kilikuwa na idadi ya wanafunzi zaidi ya elfu moja, sasa idadi hiyo imeonekana kushuka hadi wanafunzi 500 na kusababisha hofu ya hatima ya chuo hicho hali ambayo wadau wa elimu waliahidi kuandaa mikakati ya kuzuru mashinani kuzungumza na vijana ili kujiunga na chuo hicho.

Wanafunzi wa chuo cha kifundi cha Godoma eneo la Vitengeni, eneo bunge la Ganze

Maafisa tawala kwa ushirikiano na wale wa chuo hicho wakiongozwa na Afisa wa kitengo cha mauzo katika ofisi ya Katibu wa vyuo vya kiufundi Tvets, Benson Mwakima wameitikia wito wa kuzuru mashinani na kuwahamaisha vijana.

Zoezi hilo limepangwa kuanza rasmi Aprili 9 mwaka huu, ili kueleza vijana jinsi ya kutambua umuhimu wa mafunzo ya vyuo vya Tvets pamoja na kuwaeleza jinsi ya kupata mikopo ya karo kupitia bodi ya kitaifa ya elimu kuhusu mikopo, HELB.

“Tutazuru mashinani kuanza tarehe 9 mwezi Aprili na kuzungumza na wazazi na vijana wetu kuwaeleza kuhusu mafunzo ya vyuo vya kiufundi ili wajiunge na shule na suala la karo pia tutawaeleza kwa sababu hapa shuleni kwetu tunahitaji wanafunzi”, alisema Afisa wa usajali wa wanafunzi katika chuo hicho, Eric Mutai.

Mwenyekiti wa bodi ya chuo hicho Emmanuel Masha, alilalamikia hatua ya Mwalimu mkuu wa taasisi hiyo Sebastian Shikoli ya kutohudhuria mkutano huo, akisema atafanya kikao naye ili kuangizia suala hilo ikiwemo ongezeko la karo lililoibuliwa na wazazi kama changamoto kuu.

“Ni jambo la kushangaza kwamba Mwalimu mkuu hayuko kwa mkutano huu na hapa kuna masuala muhimu ambayo yanapaswa kuzungumziwa hasa suala hili la karo lakini tunajua kwamba alishikika kwa majukumu mengine, nitaongea naye, najua atakuwa ofisini wiki ijayo”, alisema Masha.

Afisa anayesimamia kituo cha polisi cha Vitengeni Mohammed Ali alisema hatua ya kuzuru mashinani na kuwahamasisha vijana waliosalia nyumbani kujiunga na vyuo vya Tvets itapunguza visa vya uhalifu mashinani.

“Tusaidiane hapa ili tufanye chuo chetu kiwe na wanafunzi na hatua hii itatusaidia sana sisi kama maafisa wa usalama kuhakikisha visa vya uhalifu vinapungua kwa sababu hawa vijana wakikaa mtaani watajihusisha na mambo maovu”, alieleza Ali.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending