Connect with us

News

Familia ya mchuuzi aliyepigwa risasi Nairobi yalilia haki.

Published

on

Familia ya Boniface Mwangi Kariuki, mchuuzi mwenye umri wa miaka 22 aliyepigwa risasi kichwani na afisa wa polisi wa kupambana na ghasia katika barabara ya Moi jijini Nairobi wakati wa maandamano sasa inaomba haki na hatua za haraka zichukuliwe.

Jonah Kariuki Nyambura babake mwathiriwa alidai hakufahamu kosa la mwanawe lililomfanya afisa wa polisi kufyatua risasi akisema alikuwa akijilinda tu kwa kuuza barakoa.

Akihutubia wanahabari Jumatano asubuhi 18 juni 2025, Nyambura alisema mwanawe yuko katika hali mahututi katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta (KNH), alikopelekwa kutibiwa baada ya kupata majeraha mabaya kichwani.

Kariuki aliongeza kuwa alifarijika baada ya kumuona mtoto wake akiwa hai, kinyume na taarifa za awali kuwa alifariki baada ya kupigwa risasi.

“Nilimuona kwenye video hiyo kwenye simu yangu, na majira ya saa nane jioni nilipigiwa simu na watu wake wa karibu kuwa mwanangu amepigwa risasi, nililala hapa (KNH) na asubuhi nilimuona katika chumba cha wagonjwa mahututi- ICU, angalau sasa nina matumaini,” alisema Kaiuku.

Aidha aliomba hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya afisa wa polisi aliyempiga risasi mwanawe.

“Ningewaomba maafisa wa polisi wawajibike kwa sababu wana watoto pia. Aliyempiga risasi pia ni mtoto wa mtu. Hatua kali zichukuliwe dhidi ya afisa huyo wa polisi,” aliongeza Kariuki.

Alikuwa ameandamana na seneta wa Busia Okiya Omtatah, ambaye alilaani ukatili wa polisi, na kuongeza kwamba tukio hilo lazima lishughulikiwe haraka.

Wakati huo huo huduma ya kitaifa ya Polisi NPS ilithibitisha kukamatwa kwa afisa aliyempiga risasi Mwangi huku shinikizo la kudhibiti ukatili wa polisi nchini likiendelea kukithiri.

Kwa upande wake rais wa chama cha mawakili Faith Odhiambo ametoa wito wa kukamatwa kwa afisa mwengine wa polisi aliyeonekana kwenye video na afisa wa polisi aliyempiga risasi mchuuzi wa barakoa kichwani wakati wa maandamano ya Jumanne 17 Juni 2025 jijini Nairobi.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending