Connect with us

News

Gachagua amtaka Rais Ruto kuangazia usalama wa Mandera

Published

on

Kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua amekosoa serikali kwa kusalia kimya kuhusiana na madai ya uwepo wa jeshi la Jubaland hapa nchini.

Naibu huyo wa rais wa zamani sasa anamtaka rais William Ruto kutoa amri ya kufurusha jeshi hilo kutoka eneo la Mandera na kurejesha hali ya usalama.

Akizungumza katika ibada ya jumapili katika kanisa la PCEA Ongata Rongai, Agosti 31, 2025, Gachagua alikashifu uvamizi huo akisema uwepo wa jeshi hilo utasambaratisha usalama mjini humo.

Vile vile alimlaumu rais Ruto akisema anachukua mda kukabiliana na ufisadi nchini suala ambalo linaendelea kurejesha nyuma maendeleo ya taifa.

“Nakusema wabunge wote kazi yao ni kuchukua hongo na hatakubali hiyo maneno, nikafurahi sana kama ameamua hivyo kwa sababu yeye mwenyewe ndiye mwenye kuhonga wabunge, nilifikiri hayo maneno ya hongo yamefika mwisho lakini sasa yameongezeka, pale ikulu ndio mahali kwa hongo na ufisadi”,alidai Gachagua

Wakati huo huo waziri wa usalama wa zamani Fred Matiang’i aliyeandamana na Gachagua aliomba wakenya kuwaunga mkono wanaoendeleza kamapeni za kumuondoa rais William Ruto mamlakani.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending