Connect with us

News

Gavana Mung’aro afutilia mbali miradi iliyokwama

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imefutilia mbali baadhi ya miradi iliyokwama ambayo ilikuwa imekabidhiwa Wanakandarasi na kushindwa kuitekeleza.

Hii ni baada ya Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Nancy Gathungu kuagiza zaidi ya kaunti 20 nchini zilizoshindwa kusimamia vyema fedha na raslimali za umma kutopewa mgao mwengine wa fedha na serikali ya kitaifa.

Kaunti hizi zinadaiwa kutotumia raslimali za umma vyema hasa wakati wa bajeti ya mwaka wa kifedha wa awali na kuchangia ofisi ya mkaguzi wa hesabu za serikali kutoa taarifa hiyo kwa umma.

Katika kikao na Wanahabari, Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro alisema baadhi ya miradi ambayo imefutiliwa mbali ni ile ya barabara za mashinani, ujenzi wa shule za Chekechea miongoni mwa miradi mingine, akisema miradi hiyo sasa itakabidhiwa wananchi kuikamilisha.

“Tumesema miradi ile ambayo wanandarasi walipewa na kaunti na wameshindwa kuitekeleza, hiyo iimefutiliwa mbali na wananchi sasa watapewa nafasi kuitekeleza, haiwezekana umepewa kazi ufanye alafu unashindwa wakati wananchi wanataka hiyo miradi kunufaika”, alisema Mung’aro.

Gavana Mung’aro alishikilia wanakandarasi waliopewa zabuni na kushindwa kuikamilisha miradi ya kaunti hawatalipwa fedha zao na miradi hiyo kukabudhiwa wanakandarasi wengine.

Akigusia suala la bills ambazo hazijalipwa, Gavana Mung’aro alidokeza kwamba kamati maalum itabuniwa ili kufuatilia suala hilo sawa na kutatua changamoto zilizopo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending