Connect with us

News

Hatma ya Gavana Mutai kuwekwa wazi na bunge la Seneti

Published

on

Kesi inayosubiriwa kwa hamu ya kumuondoa madarakani Gavana wa Kericho Erick Mutai, imeanza rasmi katika bunge la Seneti.

Kulingana na ratiba rasmi iliyotolewa na Karani wa bunge la Seneti, kikao kilitarajiwa kuanza saa tatu asubuhi kwa mkutano wa faraghani wa maandalizi ya maseneta.

Kikao hiki cha ndani kililenga kuwapa wanachama nafasi ya kupitia kanuni za mashauri na mwelekeo wa kesi kabla ya ufunguzi rasmi.

Kikao cha hadhara kilitarajiwa kuanza saa nne asubuhi kwa taratibu za awali, ikiwemo kusomwa kwa wajibu wa Seneti na utambulisho wa pande zote mbili.

Wajumbe wa Bunge la kaunti ya Kericho waliowasilisha mashtaka hayo walitambulishwa rasmi pamoja na mawakili wao.

Gavana Mutai na timu yake ya utetezi pia walitarajiwa kuwasilishwa mbele ya Baraza.

Saa tano asubuhi, mashtaka dhidi ya gavana yalisomwa, yakitoa mwelekeo wa mijadala ya siku.

Baada ya hapo kulifanyika kikao cha dakika 90 cha kushughulikia maswali na hoja za awali kabla ya kuanza kwa usikilizaji wa ushahidi.

Baada ya mapumziko ya chakula cha mchana kuanzia saa saba mchana hadi saa nane na nusu alasiri, pande zote zilipewa muda wa kutoa kauli za ufunguzi.

Bunge la kaunti, kupitia wawakilishi wake lilipewa dakika 30 kueleza hoja zake kisha timu ya utetezi ya Gavana Mutai pia iliwekewa muda wa dakika 30 kujibu.

Sehemu kubwa ya kikao cha alasiri, kuanzia saa tisa na nusu hadi saa kumi na mbili na nusu jioni, ililenga uwasilishaji wa ushahidi.

Bunge la kaunti lilitengewa muda wa saa tatu kuwasilisha mashahidi wake na kufanya upekuzi wa mahojiano.

Upande wa gavana ulipewa muda wa saa mbili kuuliza maswali ya majibu kwa mashahidi hao.

Kesi ya Gavana Mutai imevutia hisia kote nchini, si Kericho pekee, kwani itajaribu nguvu za kisiasa kati ya mabunge ya kaunti na magavana, huku ikisisitiza jukumu la kikatiba la Seneti kama msuluhishi wa migogoro ya kuondoa viongozi madarakani.

Bunge la kaunti ya Kericho limewakilishwa na mawakili 12 wakiongozwa na Elisha Ongoya. Wanaosaidia ni Kimutai Bosek, Sharon Mibey, Elias Mutuma, Hillary Kiplangat, Brian Langat, Geoffrey Langat na Victor Kibet.

Wengine ni Evans Kiplangat, Elvis Kipkorir, Joel Wakhungu na Vincent Kipronoh.

Orodha iliyowasilishwa Seneti inajumuisha maafisa wanne wa kisheria, akiwemo Brian Maingi, Ian Kiplangat, Mitchel Mutuma na Japhet Koech.

Mutai, kwa upande wake, anawakilishwa na mawakili sita wakiongozwa na Katwa Kigen, Peter Wanyama, Rose Thiong’o, Doris Ng’eno, Joash Mitei na Evanson Kirui.

Wakati wa kutoa hotuba ya utangulizi, Wakili mkuu wa Bunge la kaunti, Elisha Ongoya, aliomba kuruhusiwa kuwasilisha ushahidi mpya, jambo lililopingwa vikali na timu ya utetezi ya Mutai.

“Mheshimiwa Spika, tunapinga vikali jaribio la kuwasilisha ushahidi mpya kwa wakati huu kwa sababu hatutakuwa na nafasi ya kuupitia na kujibu kwa kuzingatia kuwa leo tumepangiwa usikilizaji wa kesi,” alisema Kigen.

Nyaraka hizo zilijumuisha vocha za malipo za idara ya kilimo, ardhi na mipango ya miji ambazo hazikuwa zimewasilishwa awali.

Pia zilikuwa na taarifa za mashahidi, barua za uhamisho wa wafanyakazi, taarifa za M-Pesa, ripoti ya kamati ya ADHOC ya kazi mtaani, rekodi za malipo na barua za kufutwa kazi miongoni mwa nyingine.

Hata hivyo, katika uamuzi wake Spika Amason Kingi aliruhusu nyaraka hizo kuwasilishwa.

“Niliposikia maelezo ya wakili wa bunge la kaunti, alibainisha kwamba nyaraka hizo ziliachwa kwa bahati mbaya wakati wa kuandaa, hazileti ushahidi mpya… kwa hivyo, kwa mujibu wa kanuni ya 30 ya taratibu za kesi, nitaruhusu nyaraka hizo kuwasilishwa,” alisema Kingi.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending