Connect with us

News

Idadi ndogo ya wapiga kura yashuhudiwa Emurua Dikkir

Published

on

Zoezi la upigaji kura katika eneo bunge la Emurua Dikkir linaendelea vyema katika vituo 94 vya kupigia kura na zoezi hilo linatarajiwa kutamatika mwendo wa saa kumi na moja unusu.

Zaidi ya wapiga kura 44,353 waliojisajiliwa wanaendelea kushiriki uchaguzi huo ili kumchagua kiongozi wanayemtaka baada ya aliyekuwa mbunge wa eneo hilo Johanna Ng’eno kufariki katika ajali ya ndege mwezi Februari mwaka huu.

Wakaazi ambao tayari wameshapiga kura, walisema umeanza vyema tangu mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi na zoezi hilo linaendelea kwa amani na usalama wa hali juu, huku wakiwataka wenzao kujitokeza na kushiriki zoezi hilo la kidemokrasia.

“Tumejitokeza toka asubuhi saa kumi na moja kupiga kura kwa amani na tunamatumiani kwamba uchaguzi utakuwa huru na haki”, alisema wakaazi.

Wakaazi wa eneo bunge la Emarua Dikkir wanashiriki uchaguzi mdogo wa eneo bunge hilo

Afisa msimamizi wa IEBC eneo bunge hilo Caleb Gikonde alisema maafisa wa tume hiyo wamejiandaa vyema kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa njia huru na haki.

“Uchaguzi unaendelea vizuri katika vituo vyote 94 katika eneo hili la Emurua Dikkir. Tumejipanga vyema na uchaguzi unaendelea, kuhakikisha watu wanashiriki uchaguzi. Wale ambao wanakuja kupiga kura tunawahimiza kubeba vitambulisho vyao”,alisema Gokonde.

Uchaguzi hao hata hivyo umewavitia zaidi ya wagombea watano, akiwemo Vincent Rotich wa Chama cha DCP, David Keter wa UDA, Desma Cherono wa PNU, Gideon Koech wa NVPK na Ken Kiprono wa RLP.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wadau wa sekta ya uchukuzi wasitisha mgomo wao

Published

on

By

Maafisa wa sekta ya uchukuzi wameahirisha mgomo wao baada ya mazungumzo yaliyoongozwa na Rais William Ruto katika ikulu ya Mombasa.

Maafisa hao wakiongozwa na rais wa Muungano wa wamiliki wa matatu Albert Karagacha wamesema kuwa mengi ya masuala waliokuwa nayo ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta nchini yameangaziwa kwa kina na rais Ruto.

Karagacha amewataka wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa umma pamoja na wamiliki wa magari ya uchukuzi wa mizigo kuhakikisha wanarudisha magari yao barabarani, akisema masuala waliowasilisha kwa rais yameangaziwa

Akizungumza mda mfupi baada ya kufanya kikao na rais William Ruto mjini Mombasa, Karagacha amesema serikali imekuwa kiangazia kwa kina masuala mbali mbali yanayohusu sekta ya uchukuzi nchini.

Aidha amesema iwapo bado serikali itakuwa inajikokota katika kufanikisha masuala waliojadiliana basi wataitisha mazungumzo zaidi na Wizara husika ili kuafikiwa kwa ajenda zao huku akisema japo suala la mzozo wa mafuta sio jambo la Kenya pekee lakini taifa inawajibu wa kusaidia wananchi wake.

Wakati huo huo Karagacha amewataka wakenya kutoingiza siasa katika suala la kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mshukiwa wa ulanguzi na usafirishaji wa watoto anyimwa dhamana

Published

on

By

Mahakama ya Shanzu imemnyima dhamana mshukiwa wa ulanguzi wa watoto zaidi ya 20.

Mahakama imeagiza mshukiwa huyo kuzuiliwa rumande ili kuwawezesha maafisa wa polisi kukamilisha uchunguzi wao.

Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa huyo Almasi Rama Amos mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa na maafisa wa upelelezi kutoka kitengo cha kupambana na ulanguzi wa binadamu na ulinzi wa watoto (AHTCPU) pamoja na maafisa wa idara ya upelelezi wa Jinai kutoka kaunti ya Mombasa.

Kukamatwa kwake kufuatia wiki kadhaa za uchunguzi kuhusu ripoti za unyanyasaji wa watoto zinazowalenga wasichana wadogo walio katika mazingira magumu.

Rama, anayetuhumiwa kwa kujihusisha na kundi linalodaiwa kuwa la ulanguzi wa watoto na dhulma za kingono na kufikishwa katika Mahakama ya Shanzu kufuatia operesheni ya kiusalama iliyoidhinishwa na maafisa hao.

Rama alipatikana katika mtaa wa Nguu Tatu eneo la Concordia katika kaunti ndogo ya Kisauni akiwa na watoto watatu wa kike.

Mahakama imeelezwa kuwa mshukiwa anadaiwa kuendesha “vituo vya uokoaji” katika kaunti za Mombasa na Kilifi kwa kujifanya kuwalea na kuwapa ushauri.

Kulingana na uchunguzi vituo hivyo vilikuwa vikitumika kama msingi wa dhulma za kingono na unyanyasaji wa watoto.

Alipokamatwa, mshukiwa aliwaongoza maafisa hadi kituo chengeni eneo la Ribe katika eneo bunge la Rabai, ambapo maafisa wa upelelezi waliwaokoa watoto 19 wa jinsia ya kike na kufikisha jumla ya waathiriwa waliookolewa kufikia ishirini na wawili (22).

Mbele ya Mahakama ya Shanzu tarehe 21 Mei, 2026, mshukiwa amekabiliwa na mfululizo wa mashtaka, ikiwemo unajisi, biashara ya watoto kwa madhumuni ya kuwadhulumu kingono pamoja na unyanyasaji wa watoto ambapo amekana mashtaka hayo.

 Kesi hiyo imepangwa kutajwa Juni 8, 2026.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending