Connect with us

News

Usalama na Elimu zavuna kwenye bajeti ya kitaifa

Published

on

Waziri wa Fedha nchini John Mbadi alisoma bajeti ya kitaifa ya mwaka wa Fedha wa 2025/2026 ambayo ni makadirio ya takriban shilingi trilioni 4.23.

Akisoma bajeti hiyo katika majengo ya bunge la kitaifa, Waziri Mbadi alisema mgao wa shilingi trilioni 3.13 ni matumizi ya kawaida ya serikali, shilingi bilioni 693.2 kwa matumizi ya maendeleo na mgao wa shilingi bilioni 474.9 ukitengewa serikali za kaunti.

Katika bajeti hiyo, Waziri Mbadi alipendekeza mgao wa shilingi bilioni 202 kwa idara ya ulinzi nchini, shilingi bilioni 125.7 kwa huduma ya usalama wa kitaifa, shilingi bilioni 51.4 zikitengwa idara ya ujasusi nchini, shilingi bilioni 32.5 kwa idara ya polisi nchini na shilingi bilioni 38.1 kwa idara ya magereza.

Waziri Mbadi alipendekeza mgao wa shilingi bilioni 138.1 kwa sekta ya Afya ili kufanikisha miradi mbalimbali ikiwemo ule wa Afya kwa wote UHC, shilingi bilioni 3.8 kwa masuala ya ardhi nchini huku shilingi bilioni 82.8 kwa sekta ya Kilimo nchini.

Waziri Mbadi, na wabunge katika majengo ya bunge la kitaifa.

Hata hivyo sekta ya elimu nchini ilitengewa mgao wa shilingi bilioni 702.7, ambapo shilingi bilioni 387.2 zimetengwa kuajiri walimu wa CBC, shilingi bilioni 5.9 kusimimia mitihani ya kitaifa, shilingi bilioni 7 kusimamia masomo ya shule za msingi, shilingi bilioni 51.9 kusimamia shule za upili na shilingi bilioni 28.9 kwa sekondari msingi.

Kulingana na Waziri Mbadi, Serikali imepunguza ushuru wa mchele kutoka nje, Wajenzi na wanaofanya kazi za ngozi wamepata afueni huku Mbadi akiongeza ushuru wa bidhaa za Anasa kama vileo Wageni wanaofanya biashara za pesa mtandaoni kulipia

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending