News
Ishmael: Tuna jukumu la kulinda maisha ya wazee katika jamii
Shirika la Kilifi Citizen Forum limekiri kwamba ukosefu wa ajira kwa vijana kaunti ya Kilifi ndio chanzo cha kuchipuka kwa visa vya mauaji ya wazee kwa tuhma za uchawi.
Afisa wa masuala ya vijana katika Shirika hilo Ishmael Jilani alisema kuna haja ya mikakati mwafaka kuidhibishwa na serikali kuu na kaunti ya Kilifi ili kudhibiti visa hivyo.
Jilani, amesema japo visa hivyo vimepungua kwa asilimia kubwa bado kuna haja ya hamasa za mara kwa mara kwa jamii mashinani pamoja na mikakati ya ajira kwa vijana kwani hatua hiyo inarudisha nyuma juhudi za maendeleo.
Aidha alidai kuchukizwa na jinsi vijana wengi wanavyowachukulia wazee kama watu wasiokuwa na thamani katika jamii, akisema wazee wana mchango kubwa hasa kwa ushauri, maarifa , hekima na pia wamekuwa mstari wa mbele katika kuelekeza serikali hasa kwenye masuala ya mipaka ya mashamba.
“Visa vya mauaji ya wazee vimetokana na vijana kukosa ajira na kutaka kutumia raslimali za wazee kujiendeleza na hapo ndio tatizo maana wazee wanahusishwa na tuhma za uchawi, tumejaribu sana kuhamasisha jamii ndiposa hivyo visa vimepungua lakini ni lazima serikali kuu na kaunti ya Kilifi kubuni ajira kwa vijana”, alisema Jilani.
Wakati huo huo aliwarai vijana kujitenga na hulka hizo na badala yake kuwa wabunifu wa ajira na kuwaheshimu wazee kwani wana mchango mkubwa kwa jamii.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

