Connect with us

News

Jamii ya Digo kaunti ya Kwale yakosoa serikali kuhusu MRC

Published

on

Jamii ya wadigo katika kaunti ya Kwale imejitokeza na kuikosoa serikali dhidi ya kauli yake kwamba kuna tetesi za kuzuka kwa vuguvugu la Mombasa Repubilican Council MRC.

Jamii hiyo ikiongozwa na Balozi Chirau Ali Mwakwere ilisema kauli hiyo ya serikali inalenga kuchangia uzushi na wasiwasi kwa jamii hiyo, kwani kuna njama za kuzuka kwa vuguvugu la MRC.

Balozi Mwakwere, alisema jamii ya wadigo haiungi mkono vuguvugu la MRC na iwapo serikali iko na taarifa zozote kuhusu kauli hizo basi iwaeleze wananchi ili wafahamu na wala sio kuchangia uzushi na wasiwasi kwani kauli hizo huenda zikaathiri sekta ya utalii.

“Tulishangaa kabisa kusikia serikali ikisema hivyo kwa sababu huo ni uzushi na imetutia wasiwasi sana kwenye familia zetu, watoto wetu, sisi wazee, wake kwa waume, kwa sababu hakuna MRC hiyo iliisha zamani, sasa serikali inasema imeanza tena, twaiomba serikali itwambie imeanza tena ni akina nani?”,aliuliza Mwakwere.

Jamii hiyo hata hivyo iliweka wazi kwamba haitakubali kuhusishwa na makundi ambayo hayana msingi wowote kwa wananchi.

“Mwataka kutwambai sisi wanawake wa Kidigo twazaa visirani? Sisi hatujazaa visirani, ielekeweke hivyo hatujazaa na wala hatutazaa visirani. Sisi kama kama magen z wa hapa ndani ya Kwale hatukufanya vurugu la aina yeyote leo tunakuaje sisi ni MRC au kwa sababu sisi niwanyonge?”,walisema wakaazi hao.

Kauli zao zilijiri baada ya serikali kupitia kaunti ya kamishna wa kaunti ya Kwale Stephen Orinde kusema kwamba kuna taarifa za kijasusi za kuchipuka kwa vuguvugu la kundi la MRC ambalo linalenga kutatizo usalama wa kaunti ya Kwale.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending