Connect with us

News

Kampeni za uchaguzi mdogo zatamatika rasmi

Published

on

Kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge, useneta na uwakilishi wadi katika maeneo mbalimbali, zinatarajiwa kutamatika rasmi siku ya Jumatatu Novemba 24 mwaka huu wa 2025, saa kumi na mbili jioni.

Hii ni baada ya Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kupitia Mwenyekiti wake Erastus Ethekon kutangaza kipindi cha kampeni kuanza Oktoba 8 hadi Novemba 24 na kwamba zinafaa kufanyika kwa amani.

Katika kampeni hizo za lala salama kabla ya dirisha la kampeni kufungwa rasmi na Tume ya IEBC, viongozi mbalimbali ikiwemo wale wa Serikali na upinzani walionekana kuonyeshana ubabe wa kisiasa katika kampeni hizo.

Wazee wa Kaya za mijikenda katika eneo la Pwani, Wakiongozwa na Mratibu wa Wazee hao Tsuma Nzai Kombe, wameitaka Tume ya IEBC kuhakikishia chaguzi hizo zinakuwa huru na haki ili kudumisha amani nchini.

“Sisi kama wazee wa Kaya tunataka uchaguzi uwe huru na haki na maafisa wa IEBC wahakikisha wanaandaa uchaguzi wa amani ili kila mmoja awe na haki ya kuchagua kiongozi anayemtaka. Hapa Magarini tunataka amani na sio vurugu kwa sababu watu wenyewe wa Magarini wanapenda amani”, walisema wazee hao.

Kamishna wa IEBC Alutalala Mukhwana amewahakikishia wakenya uchaguzi huru na haki huku akionya kuchukuliwa hatua za kisheria kwa viongozi wanaolenga kuzuru vurugu wakati wa uchaguzi.

“Sisi kama IEBC tumejipanga na tunawaambia watu wa Magarini na kwengine ambako uchaguzi utafanyika kwamba utakuwa huru na haki na maafisa wote wamepewa mafunzo kuhakikisha unatekeleza majukumu yao vyema”, alisema Alutalala.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending