News
Kanisa lamtaka Rais Ruto kuipa uhuru tume ya EACC
Viongozi wa makanisa wanamtaka rais William Ruto kutimiza vitisho vyake na kuwachukulia hatua wabunge anaodai wanahusika na visa vya ufisadi nchini.
Baraza la makanisa nchini NCCK likiongozwa na naibu mwenyekiti wake Askofu John Okinda akizungumza wakati wa ibada eneo la Roisambu, alimtaka Rais William Ruto kuwasilisha Ushahidi dhidi ya wabunge wanaokula hongo ili wakamatwe.
Pia alimtaka rais William Ruto kuipa tume ya kukabili ufisadi nchini EACC jukumu huru la kufanya kazi yake.
Wakati huo huo muungano mpya wa Kenya Moja ulirai vyama vya upinzani kushikana mkono nao ili kuibandua mamlakani serikali ya rais William Ruto katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.
Wakiongozwa na seneta wa kaunti ya Nairobi Edwin Sifuna, mrengo huo wa viongozi wachanga, uliapa kuendelea kusukuma wimbi jipya la wanasiasa wanaopinga sera za Kenya Kwanza.
Hata hivyo baadhi ya mawaziri nchini walijitokeza na kuwasuta wabunge wanaodai kwamba watawasilisha mswada bungeni wa kumtimua rais William Ruto mamlakani kutokana na kauli yake kwamba wabunge ni wafisadi.
Waziri wa kawi na nishati nchini Opiyo Wandayi aliwataka wabunge kusitisha mchakato huo na kujidhihirisha wazi kwa umma kama wao sio wafisadi.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

