Connect with us

News

Kanja: Polisi kuwasaka mawakala tapeli wa ajira za ughaibuni

Published

on

Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja amesema uchunguzi unaendelea ili kuwatambua mawakala matapeli waliowahadaa wakenya kujiunga na jeshi la Urusi kupigana vita dhidi ya Ukraine.

Akizungumza mjini Mombasa katika Kongamano la usalama, Kanja alisema maafisa wa Idara ya upelelezi wa makosa ya Jinai, DCI, tayari wameanzisha uchunguzi wa kina kuhusu sakata hiyo.

Aidha alionya kwamba yeyote atakayepatikana na hatia atachukuliwa hatua kali za kisheria na kufikishwa Mahakamani, akieleza wasiwasi wake kuhusu ongezeko la visa vya uhalifu vinavyohusishi baadhi ya wahudumu wa bodaboda.

Afisa huyo mkuu wa polisi nchini aliwataka wahudumu badoboda kujisajili katika makundi au vyama vinavyotambulika kisheria ili kurahisisha utambuzi wao na kudhibiti wale wanaotumia sekta hiyo kama kisingizio cha kutekeleza uhalifu.

Aidha, aliwaonya vijana wanaojihusisha na magenge ya kihalifu maarufu kama Panga boys, akisisitiza kuwa Jeshi la Polisi halitavumilia vitendo vya aina hiyo.

Wakati huo huo alisema kwamba maafisa wa usalama watachukua hatua madhubuti dhidi ya wahalifu wote ili kulinda maisha na mali ya wananchi.

Kanda na hayo, Afisa huyo wa mkuu wa polisi aliongeza kwamba kadri taifa linajiandaa kwa uchaguzi mkuu, vyombo vya usalama vinaendelea kubuni na kuimarisha mikakati ya kuhakikisha taifa linashuhudia amani, utulivu na usalama.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending