Connect with us

News

Karua, Aomba Mahakama Kumuachilia Bessigye kwa Dhamana

Published

on

Kiongozi wa Chama cha People’s Liberation Party, PLP nchini Kenya Martha Karua, aliwasili nchini Uganda katika juhudi za kumuakilisha Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Bessigye anayetuhumiwa kwa kosa la Uhaini.

Bessigye alikamatwa nchini Kenya miezi sita iliyopita na kuwasilishwa Mahakamani licha ya hali yake ya kiafya kuonekana kudhoofika.

Akiwasilisha hoja yake Mahakamani, Karua ameitaka Mahakama hiyo kumuwachilia Bessigye kwa dhamana ikizingatiwa kwamba amekuwa akizuiliwa kwa zaidi ya siku 180 korokoroni bila ya kupata haki.

Kinyume na matukio ya hivi majuzi nchini Tanzania ambako alizuiliwa kwa muda wa saa sita na kisha kurejeshwa nchini Kenya, Kiongozi huyo chama cha PLP, alilakiwa Mahakamani kwa shangwe na nyimbo za ukombozi, kabla ya kupewa nafasi na Mahakama kuwasilisha hoja yake.

Safari yake ya kwenda nchini Uganda kuhudhuria kesi hiyo, inatokea wiki mbili tu baada ya kutibuka kwa jaribio lake la kutaka kumuakilisha kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu, ambapo yeye na Wanaharakati wengine wa haki za binadamu walizuiliwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kabla ya kurejeshwa nchini Kenya.

Tukio hilo limezua mashambulio makali ya mitandaoni miongoni mwa kizazi cha sasa cha Gen Z kuishtumu Tanzania kwa madai ya kudhuliwa kwa Mwanaharakati Bonifance Mwangi na mwenzake Agathar Atuhaire kutoka nchini Uganda.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi yawatupa gerezani washtakiwa zaidi ya 10

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa washtakiwa zaidi ya 10 waliowasilishwa Mahakamani wakikabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwemo kesi za unajisi na makosa ya jinai.

Katika vikao vya Mahakama siku ya Jumatano tarehe 3 June 2026, Hakimu Ivy Wasike ametoa hukumu hizo kwa watuhumiwa hao huku wengine wakifungwa kwa zaidi ya miaka 30 gerezani.

Simon Ngala, Aliwali Ali Mwalimu, Christopher Buru, miongoni mwa wengine zaidi ya 10 walifikishwa katika Mahakama ya Kilifi na kuhukumiwa kufuatia mashtaka mbalimbali yanayowakabili ikiwemo mashtaka ya unajisi na makosa ya jinai.

Hakimu wa Mahakama ya Kilifi Ivy Wasike, alimhukumu kifungo cha miaka 30 gerezani Simon Ngala baada ya kupatikana na hatia ya kumnajisi mtoto wa miaka 13 kisha akamtorosha kwao kwa kipindi cha mwezi mzima.

Mwengine ni Aliwali Ali Mwalimu, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 25 kufuatia mashtaka ya kumpachika ujauzito mtoto wa miaka 13 licha ya kuomba msamaha Mahakamani.

Wakati wa kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisikitishwa na kukithiri kwa visa vya watoto kupotea na kisha kunajisiwa katika kaunti ya Kilifi.

Kiongozi wa mashtaka katika Mahakama hiyo Nancy Njeru alipinga vikali ombi lililowasilishwa Mahakama la kutaka washtakiwa wasamehewe, kwanin wengine walidai kwamba walishirika makosa hayo bila kukusudia, akisema hukumu hizo zitakuwa funzo kwa watu wenye hulka hizo katika jamii.

Mbali na hukumu za kesi za unajisi, Christopher Buru alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani akikabiliwa na mashtaka ya wizi baada ya kupatikana na hatia ya kutumia pesa za mlalamishi Saumu Nyevu aliyekuwa akimtumia pesa alipokuwa akifanya kazi katika milki za kiarabu, kosa lililomchukiza zaidi Hakimu Wasike.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Washukiwa 5 wa uhalifu wanazuiliwa na polisi Likoni

Published

on

By

Maafisa wa polisi katika eneo bunge la Likoni kaunti ya Mombasa wanawazuiliwa washukiwa 5 wa uhalifu waliokamatwa katika oparesheni iliyofanyika maeneo ya Duduz na Bufallo siku ya Jumatatu tarehe mosi Juni 2026.

Washukiwa waliokamatwa ni Brian Musa mwenye umri wa miaka 24, Abubakar Mahasi wa umri wa miaka 20, Juma Kassim mwenye umri wa miaka 16, Omar Gobeko maarufu Mboga mwenye umri wa miaka 19 na Jackson Mwambu mwenye umri wa miaka 26.

Msako huo uliongozwa na mkuu wa kituo cha polisi cha Shelly Beach pamoja na kikosi cha maafisa wa polisi.

Maafisa wa Polisi wamesema mshukiwa Brian Musa anakabiliwa na tuhuma za maandalizi ya kutenda kosa la jinai, huku Ababakar Mahasi, Juma Kassim na Omar Gobeko wakihusishwa na tuhuma za wizi wa mabavu.

Mshukiwa mwengine Jackson Mwambu anahusishwa na tuhuma za kupatikana na mali ya serikali kinyume cha sheria.

Katika oparesheni hiyo, maafisa wa polisi walifanikiwa kupata vielelezo mbali mbali ikiwemo panga tatu pamoja na koti la jeshi la KDF.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending