Connect with us

News

Kenya na Ufaransa zimetia saini mikataba ya bilioni 104

Published

on

Kenya na Ufaransa zimetia saini makubaliano ya kuanzisha ubia wa usafirishaji na maendeleo ya miundombinu ya bandari inayokadiriwa kuwa takribani shilingi bilioni 104.

Makubaliano mengine yanahusu uzalishaji endelevu wa mafuta ya anga, ushirikiano wa kiuchumi wa majini.

Nchi hizo mbili zilikubali zaidi kukuza mauzo ya majani chai ya Kenya kwa masoko ya Ufaransa na kuimarisha ushirikiano katika huduma za afya, elimu na mafunzo ya kiufundi.

Akizungumza wakati wa kutia saini makubalaiano hayo, rais Wiliam Ruto amesema Kenya inalenga kunufaika na utaalamu wa Ufaransa katika nishati ya Nyuklia huku nchi hiyo ikifuatilia lengo lake la kuzalisha megawati 10,000 za umeme.

Rais Ruto ameongeza kuwa Kenya na Ufaransa zimejadili jinsi ya  kuboresha muunganisho wa anga ili kusaidia biashara, utalii na uwekezaji.

Kwa upande wake rais wa ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi yake inasalia na nia ya kupanua uwekezaji na ushirikiano kote barani Afrika na kusaidia mageuzi katika mfumo wa fedha wa kimataifa.

Hata hivyo viongozi wanahudhuria Kongamano la la siku mbili la Afrika ambapo zaidi ya marais 30 kutoka bara la Afrika pamoja na wajumbe elfu tatu kutoka mataifa mbalimbali pia nao wko humu nchini kuhudhuria Kongamano hilo. 

Kongamano hilo linafanyika katika ukimbi wa mikutano wa KICC jijini Nairobi, linalenga kuangazia masuala ya muhimu ya kanda ya Afrika.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mbunge wa Nyali amepuzilia mbali madai ya kuhusishwa na siasa za ukabila

Published

on

By

Mbunge wa Nyali kaunti ya Mombasa Mohamed Ali amepuzilia mbali madai ya kuhusishwa na siasa za ukabila kwenye kaunti hiyo, akisema anafanya siasa zake bila kujali dini, kabila au hata eneo.

Akizungumza huko Nyali, Ali alisema kuna baadhi ya viongozi katika kaunti ya Mombasa, ambao wamekuwa wakiendekeza propaganda za kumhusisha na siasa za migawanyiko ili kumharibia jina taifa linapojiandaa kwa uchaguzi mkuu ujao wa 2027.

Ali ambaye alitangaza kuwania wadhifa wa ugavana kaunti ya Mombasa, aliwataka viongozi kufanya siasa zao kwa kunadi sera zao kwa wakaazi na maendeleo ambayo watatekeleza na sio kutumia suala la ukabila kuwachafulia wengine jina.

“2017 hakuna mtu aliniita mkabila, 2022 hakuna mtu aliniita mkabila, 2027 wanasema Mohamed Ali ni mkabila.Mimi Mohamed Ali, mimi nauliza nikisimama hapa juu ya gari, niseme kabila zote za Kenya wanaweza pewa nafasi ya ugavana ni kuna makosa?,basi sasa wanazunguka wakisema Mohamed ni mkabila kwasababu ameanza kufungua watu macho’’ alisema Ali.

Aidha, Ali alisema ataendelea kuzuru maeneo mbalimbali ya kauti ya Mombasa kunadi sera zake na kuwataka wakaazi wa kaunti hiyo kuwachagua viongozi wanaofaa ambao wataimarisha kaunti hiyo kimaendeleo.

‘’Mimi nimewaambia nitatembea hii Mombasa kwa uwezo wake mwenyezi mungu kutetea wananchi wa Mombasa’’ aliongeza Ali

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Wakimbizi nusu milioni wakabiliwa na baa la njaa, Dadaab

Published

on

Ripoti iliyotolewa hivi karibu na Shirika la Chakula duniani WFP ilionyesha kwamba zaidi ya wakimbizi nusu milioni wanaoishi katika kambi za wakimbizi za Kakuma na Dadaab zilizoko nchini Kenya, wako katika hatari ya kuangamia kutokana na baa la njaa.

Kambi hizi ambazo zinahifadhi wakimbizi wengi zaidi kutoka nchini Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Somalia, ziko hatari iwapo zitakosa misaada ya chakula.

Kufuatia hali hiyo ambayo pia imechangiwa na mashirika ya kimataifa kusitisha ufadhili, sasa hali huenda ikawa tofauti baada ya taifa la Korea kwa ushirikiano na Kenya kutoa ufadhili wa shehena ya nafaka ya zaidi ya tani elfu 10 ambayo inakadiriwa kuwa kima cha shilingi milioni 1.2.

Katibu katika Idara ya uhamiaji nchini Belio Kipsang, aliyepokea msaada huo wa Chakula mjini Mombasa na kuhifadhiwa katika maghala ya Shirika la WFP, ameonya kwamba iwapo Kenya itakosa kupokea msaada kutoka kwa washirika na wafadhili wengine, basi italazimika kuchukua maamuzi magumu, ikiwemo kuwaondoa baadhi ya wakimbizi.

“Nyuma ya kila takwimu kuna familia ambazo ustahimilivu wao unaendelea kujaribiwa kila siku: akina mama wanaokosa kula ili watoto wao wapate chakula, watu walio katika mazingira hatarishi wakiruka milo, na vijana wanaokabiliwa na mustakabali usio na uhakika. Hizi si takwimu za kufikirika. Zinawakilisha watu halisi ambao heshima yao, afya yao na matarajio yao ya maisha yanategemea maamuzi tunayofanya kwa pamoja,” alisema.

Wakati wa hafla hiyo ya kupokea msaada huo wa chakula kwa wakimbizi wa Kakuma na Dadaab, Mkurugenzi wa Shirika la WFP nchini Kenya Betty Ka, alisema shehena ya nafaka itasaidia kuwahudumia takribani wakimbizi nusu milioni katika miezi ijayo.

“Usafirishaji huu unaonyesha umuhimu wa ushirikiano imara katika mnyororo wa ugavi wa misaada ya kibinadamu, ambapo ushirikiano huu kati ya Kenya, Mamlaka ya bandari Kenya (KPA), Shirika la viwango la Kenya(KEBS) na mpango wa Chakula Duniani (WFP) kwa kuhakikisha kwamba chakula cha msaada kinafanikishwa”,alisema Betty.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending