News
Mahakamani ya Shanzu yamzuia kwa siku 14 mshukiwa wa mauaji ya Keziah
Mahakamani ya Shanzu imeagiza kuzuiliwa kwa siku 14 kwa mshukiwa wa mauaji ya mtoto Keziah Matuki, aliyekuwa na umri wa miaka 7.
Mahakama imetoa agizo hilo baada ya maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai DCI kuiomba Mahakama kuwapa muda zaidi wa kukamilisha uchunguzi wao na kuwasilisha ushahidi Mahakamani.
Maafisa hao wamesema wanataka muda zaidi ili kukamilisha uchunguzi wao, ambapo mshukiwa atafanyiwa vipimo vya DNA katika maabara ya serikali, kuhojiwa zaidi kuhusu tukio hilo, pamoja kuwasilishwa kwa ripoti ya madaktari ya upasuaji wa miati Mahakamani.
Mshukiwa huyo kwa jina Dennis Otieno Oduor kwa jina maarufu Dennis Mkikuu Mwobolo, anadaiwa kutekeleza kitendo hicho cha kinyama kwa mtoto huyo ikiwa ni pamoja na kumnajisi na kumnyonga na kisha kumvunja shingo.

Mshukiwa wa mauaji ya mtoto Keziah, Dennis Otieno Oduor kwa jina maarufu Dennis Mkikuu Mwobolo, afikishwa katika Mahakama ya Shanzu
Tukio hilo linadaiwa kutekelezwa mnamo tarehe 3 mwezi Mei mwaka huu katika kijiji cha Kwa Nzai eneo la Mwezang’ombe kaunti ya Kilifi.
Kesi hiyo itatajwa tena mnamo tarehe 25 mwezi Mei mwaka huu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

