Connect with us

News

Afrika Forward Summit inahitaji trilioni 11 kufadhili Kilimo Afrika

Published

on

Licha ya Afrika kuwa na takribani asilimia 60 ya ardhi isiyotumika kwa shughuli za Kilimo bado inakabiliwa na pengo kubwa la ufadhili wa Kilimo kwa zaidi ya shilingi trilioni 11 kila mwaka.

Wataalam wanasema hali hiyo inadidimiza uzalishaji wa chakula, ukuaji wa biashara za Kilimo na uundaji wa ajira.

Swala hilo limesababisha viongozi wa Afrika, taasisi za kifedha pamoja na wadau mbalimbali wa kimataifa kuweka azimio jipya la kuimarisha ufadhili wa Kilimo barani Afrika.

Hata hivyo utiaji wa saini wa suala hilo itakuwa ni kilele cha Kongamano la Afrika Forward Summit inalofanyika jijini Nairobi na ambalo linafadhiliwa na serikali ya Kenya na Ufaransa.

Kongamano hilo linatarajiwa kutamatika leo, tarehe 12 Mei 2026 huku masuala mbalimbali muhimu ikiwemo uboreshaji wa kimaendeleo, uwekezaji wa kikanda na ukuaji wa kiuchumi yakiangaziwa.

Kongamano la Afrika Forward Summit inafanyika jijini Nairobi na kuhudhuriwa na marais 30 kutoka mataifa ya bara la Afrika

Wanaharakati zaidi ya 100 waliohudhuria Kongamano hilo waliwasilisha mapendekezo yao kwa viongozi hao wa Afrika, wakitaka kulindwa kwa raslimali za Afrika ikiwemo Madini, kupanuliwa kwa uhuru wa kibiashara kati ya mataifa ya Afrika na kuboreshwa kwa mifumo ya utawala na demokrasia.

Tayari Kenya na Ufaransa zimetia saini makubaliano ya kuanzisha ubia wa usafirishaji na maendeleo ya miundombinu ya bandari inayokadiriwa kuwa takriban shilingi bilioni 104.

Makubaliano mengine yanahusu uzalishaji endelevu wa mafuta ya ndege, na ushirikiano wa uchumi wa majini.

Nchi hizo mbili zilikubaliana pia kukuza mauzo ya majani Chai maalum ya Kenya kwa masoko ya Ufaransa na kuimarisha ushirikiano katika huduma za afya, elimu na mafunzo ya kiufundi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending