Connect with us

News

Afrika Forward Summit inahitaji trilioni 11 kufadhili Kilimo Afrika

Published

on

Licha ya Afrika kuwa na takribani asilimia 60 ya ardhi isiyotumika kwa shughuli za Kilimo bado inakabiliwa na pengo kubwa la ufadhili wa Kilimo kwa zaidi ya shilingi trilioni 11 kila mwaka.

Wataalam wanasema hali hiyo inadidimiza uzalishaji wa chakula, ukuaji wa biashara za Kilimo na uundaji wa ajira.

Swala hilo limesababisha viongozi wa Afrika, taasisi za kifedha pamoja na wadau mbalimbali wa kimataifa kuweka azimio jipya la kuimarisha ufadhili wa Kilimo barani Afrika.

Hata hivyo utiaji wa saini wa suala hilo itakuwa ni kilele cha Kongamano la Afrika Forward Summit inalofanyika jijini Nairobi na ambalo linafadhiliwa na serikali ya Kenya na Ufaransa.

Kongamano hilo linatarajiwa kutamatika leo, tarehe 12 Mei 2026 huku masuala mbalimbali muhimu ikiwemo uboreshaji wa kimaendeleo, uwekezaji wa kikanda na ukuaji wa kiuchumi yakiangaziwa.

Kongamano la Afrika Forward Summit inafanyika jijini Nairobi na kuhudhuriwa na marais 30 kutoka mataifa ya bara la Afrika

Wanaharakati zaidi ya 100 waliohudhuria Kongamano hilo waliwasilisha mapendekezo yao kwa viongozi hao wa Afrika, wakitaka kulindwa kwa raslimali za Afrika ikiwemo Madini, kupanuliwa kwa uhuru wa kibiashara kati ya mataifa ya Afrika na kuboreshwa kwa mifumo ya utawala na demokrasia.

Tayari Kenya na Ufaransa zimetia saini makubaliano ya kuanzisha ubia wa usafirishaji na maendeleo ya miundombinu ya bandari inayokadiriwa kuwa takriban shilingi bilioni 104.

Makubaliano mengine yanahusu uzalishaji endelevu wa mafuta ya ndege, na ushirikiano wa uchumi wa majini.

Nchi hizo mbili zilikubaliana pia kukuza mauzo ya majani Chai maalum ya Kenya kwa masoko ya Ufaransa na kuimarisha ushirikiano katika huduma za afya, elimu na mafunzo ya kiufundi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wadau wa sekta ya uchukuzi wasitisha mgomo wao

Published

on

By

Maafisa wa sekta ya uchukuzi wameahirisha mgomo wao baada ya mazungumzo yaliyoongozwa na Rais William Ruto katika ikulu ya Mombasa.

Maafisa hao wakiongozwa na rais wa Muungano wa wamiliki wa matatu Albert Karagacha wamesema kuwa mengi ya masuala waliokuwa nayo ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta nchini yameangaziwa kwa kina na rais Ruto.

Karagacha amewataka wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa umma pamoja na wamiliki wa magari ya uchukuzi wa mizigo kuhakikisha wanarudisha magari yao barabarani, akisema masuala waliowasilisha kwa rais yameangaziwa

Akizungumza mda mfupi baada ya kufanya kikao na rais William Ruto mjini Mombasa, Karagacha amesema serikali imekuwa kiangazia kwa kina masuala mbali mbali yanayohusu sekta ya uchukuzi nchini.

Aidha amesema iwapo bado serikali itakuwa inajikokota katika kufanikisha masuala waliojadiliana basi wataitisha mazungumzo zaidi na Wizara husika ili kuafikiwa kwa ajenda zao huku akisema japo suala la mzozo wa mafuta sio jambo la Kenya pekee lakini taifa inawajibu wa kusaidia wananchi wake.

Wakati huo huo Karagacha amewataka wakenya kutoingiza siasa katika suala la kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mshukiwa wa ulanguzi na usafirishaji wa watoto anyimwa dhamana

Published

on

By

Mahakama ya Shanzu imemnyima dhamana mshukiwa wa ulanguzi wa watoto zaidi ya 20.

Mahakama imeagiza mshukiwa huyo kuzuiliwa rumande ili kuwawezesha maafisa wa polisi kukamilisha uchunguzi wao.

Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa huyo Almasi Rama Amos mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa na maafisa wa upelelezi kutoka kitengo cha kupambana na ulanguzi wa binadamu na ulinzi wa watoto (AHTCPU) pamoja na maafisa wa idara ya upelelezi wa Jinai kutoka kaunti ya Mombasa.

Kukamatwa kwake kufuatia wiki kadhaa za uchunguzi kuhusu ripoti za unyanyasaji wa watoto zinazowalenga wasichana wadogo walio katika mazingira magumu.

Rama, anayetuhumiwa kwa kujihusisha na kundi linalodaiwa kuwa la ulanguzi wa watoto na dhulma za kingono na kufikishwa katika Mahakama ya Shanzu kufuatia operesheni ya kiusalama iliyoidhinishwa na maafisa hao.

Rama alipatikana katika mtaa wa Nguu Tatu eneo la Concordia katika kaunti ndogo ya Kisauni akiwa na watoto watatu wa kike.

Mahakama imeelezwa kuwa mshukiwa anadaiwa kuendesha “vituo vya uokoaji” katika kaunti za Mombasa na Kilifi kwa kujifanya kuwalea na kuwapa ushauri.

Kulingana na uchunguzi vituo hivyo vilikuwa vikitumika kama msingi wa dhulma za kingono na unyanyasaji wa watoto.

Alipokamatwa, mshukiwa aliwaongoza maafisa hadi kituo chengeni eneo la Ribe katika eneo bunge la Rabai, ambapo maafisa wa upelelezi waliwaokoa watoto 19 wa jinsia ya kike na kufikisha jumla ya waathiriwa waliookolewa kufikia ishirini na wawili (22).

Mbele ya Mahakama ya Shanzu tarehe 21 Mei, 2026, mshukiwa amekabiliwa na mfululizo wa mashtaka, ikiwemo unajisi, biashara ya watoto kwa madhumuni ya kuwadhulumu kingono pamoja na unyanyasaji wa watoto ambapo amekana mashtaka hayo.

 Kesi hiyo imepangwa kutajwa Juni 8, 2026.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending