Connect with us

News

Kenya, Ufaransa kukabili mabadiliko ya tabia nchi.

Published

on

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesisitiza ushirikiano kati ya ufaransa na Kenya katika kutetea ajenda ya kimataifa inayojumuisha maendeleo endelevu na hatua za kukabili mabadiliko ya tabia nchi, kabla ya mkutano mwengine utakaohusisha bara afrika na Ufaransa jijini Nairobi mwaka ujao.

Akizungumza kutoka Seville katika kongamano la ngazi ya juu kuhusu ushirikiano wa kimataifa, Rais Macron alisisitiza maono yake ya pamoja na Rais William Ruto akisema hakuna nchi inapaswa kulazimishwa kuchagua kati ya maendeleo ya kiuchumi na ulinzi wa mazingira.

“Pamoja na Rais William Ruto, tunashiriki ahadi moja: kwamba hakuna nchi inapaswa kuchagua kati ya maendeleo na kulinda sayari,” Macron alisema. “Haya ndiyo matamanio tunayoleta leo Seville na washirika wetu, kama sehemu ya mkataba wa mafanikio, watu na sayari uliozinduliwa miaka miwili iliyopita huko Paris.”

Viongozi hao wawili wanatarajiwa kuendeleza ajenda hii katika kongamano la Afrika na Ufaransa 2026, ambalo litasimamiwa na Kenya na Ufaransa jijini Nairobi.

Mkutano huo unatazamiwa kuangazia ushirikiano wa kibunifu unaoshughulikia malengo ya maendeleo endelevu ya afrika sambamba na kukuza ukuaji wa uchumi jumuishi.

Rais Macron pia alisema kuwa Kenya na Ufaransa zinashirikiana kikamilifu katika miradi muhimu ya nchi mbili kama vile mpito wa nishati, miundombinu endelevu ya uchukuzi na maendeleo ya kilimo.

Alisema miradi hii, inaonyesha aina ya ushirikiano wa kimantiki unaohitajika ili kufikia maendeleo yanayostahimili hali ya hewa.

Mbali na ushirikiano wa kiuchumi na kimazingira, marais hao wawili walisisitiza dhamira yao ya pamoja ya kukuza amani na usalama kote barani Afrika, hasa katika eneo la Maziwa Makuu, Sudan na Somalia.

“Tulisisitiza dhamira yetu ya pamoja ya amani na usalama katika eneo la Maziwa Makuu, Sudan, na Somalia,” Rais Macron alibainisha, akisisitiza jukumu la Ufaransa na Kenya kusaidia utulivu wa kikanda kupitia ushirikiano wa kidiplomasia na usaidizi wa maendeleo.

Tarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending