News
Kenya yaadhimisha miaka 15 ya Katiba
Kenya inaadhimisha miaka 15 ya Katiba mpya tangu kubuniwa rasmi mwaka wa 2010 chini ya utawala wa Hayati Mwai Kibaki kufuatia shinikizo la miaka mingi ya mifumo ya majimbo yaliyoanzishwa na Marehemu Ronald Ngala wakati wa utawala wa Hayati Mzee Jomo Kanyatta.
Shinikizo hizo hazikuishia wakati huo licha ya kuzongwa na siasa za kibepare, Mwanasiasa Raila Odinga wakati huo alianzisha vuguvugu la vyama vingi na kuchangia kuyumbishwa kwa mpango huo na kupelekea utawala wa Rais wa pili wa Kenya Hayati Daniel Arap Moi kuruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka wa 1992.
Kutokana na kwamba wakenya walikuwa na nia ya kushuhudia mabadiliko nchini na uhuru wa kujieleza, walianzisha kura ya maoni yani ‘Referendum’ na kuafikia kubuniwa kwa katiba mpya mwaka wa 2010.
Kubuniwa kwa Katiba hiyo mpya kulichangia mabadiliko mengi nchini ya kiuongozi, kielimu, huru wa kujieleza, kuandamana na demokrasia ya taifa kote nchini.
Mnamo Agosti 25, 2025 Rais William Ruto alitangaza kwamba Agosti 27, itakuwa siku ya kitaifa ya Katiba Dei ambayo itakuwa ikiadhimishwa kila mwaka.
Tangazo hilo la rais lilifafanua zaidi kwamba siku hiyo itakuwa siku ya kawaida ya kazi na wala sio siku ya kitaifa ya mapumziko na kwamba itawawezesha wakenya kufahamu masuala mbalimbali ya Katiba, utawala wa sheria na mazungumzo ya kitaifa.

Rais William Ruto akitia saini sheria mpya kuhusu Katiba Dei kama siku ya kitaifa
Aidha lengo kuu la Katiba Dei ni kuangazia safari ya kidemokrasia ya Kenya na kuhimiza haki ya umma katika mijadala mbalimbali ya utawala kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali kote nchini.
Hata hivyo himizo zaidi ni kwa mihimili tatu ya serikali, ngazi zote mbili za kiutawala na taasisi za kielimu zitahitajika kuandaa na kushiriki katika shughuli za umma ili kukuza uelewa wa Katiba na ushirikishwaji wa umma.
Baadhi ya wakenya walisema licha ya Katiba ya Kenya kutimiza miaka 15 tangu kubuniwa rasmi, viongozi wengi wanaonekana kutozingatia muongozo wa Katiba hiyo sawa na kanuni zake huku wakisema kwamba ni muhimu kwa kila mmoja wakiwemo viongozi kuwajibika na kuhakikisha wanatekeleza ahadi zao kwa mujibu wa kanuni na sheria za Katiba.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

