Connect with us

News

Kesi ya Pembe za Ndovu kuendelea katika Mahakama ya Mombasa

Published

on

Raia wawili wa taifa la Burundi wamefikishwa katika Mahakama ya Mombasa kwa madai ya kumiliki na kujaribu kusafirisha pembe za Ndovu zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 12.

Gakiza Sulemani na Nkunubumwe Celecius walifikishwa mbele ya Hakimu mkaazi Mwandamizi David Odhiambo kwa makosa ya kushughulikia vipande 27 vya pembe za Ndovu kinyume cha sheria.

Pembe hizo zilizokadiriwa kuwa na uzito wa kilo 62.85, zilinaswa katika eneo la Miritini kaunti ya Mombasa kufuatia operesheni ya kijasusi iliyotekelezwa na maafisa wa Huduma ya Wanyamapori nchini KWS.

Washukiwa hao pia walikabiliwa na shtaka la pili la kumiliki sehemu za wanyamapori walioko kwenye hatari ya kutoweka bila idhini ya serikali kinyume na sheria ya mwaka 2013.

Washukiwa hao hata hivyo walikana mashtaka hayo huku Mahakama ikiwaachilia kwa dhamana ya shilingi milioni 4 kila mmoja na mdhamini wa kiasi sawa na hicho pamoja na masharti ya kuwasilisha pasipoti zao na majina ya Wakenya wawili wa kuwawajibikia.

Kesi hiyo itatajwa tena mnamo tarehe 20 mwezi huu Agosti.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending