News
Kindiki, aendeleza mpango wa Wezesha jamii Taveta
Naibu Rais Prof Kithure Kindiki ameahidi kuendeleza mpango wa Wezesha jamii maarufu Economic Empowerment Programme maeneo mbalimbali kote nchini.
Akizunguza katika kaunti ya Taita taveta wakati wa halfa hiyo, Kindiki amesema serikali itahakikisha wananchi wanakabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi nchini.
Kindiki ambaye aliambatana na viongozi wengine wa Kenya Kwanza, akiwemo mbunge wa Kapseret Osacar Sudi wameushtumu upande wa upinzani wakisema hawana ajenda maalum.
Waziri wa madini na raslimali za baharini nchini Ali Hasan Joho alieleza azma yake ya kuwania wadhfa wa urais ifikapo mwaka 2032 huku akisema kwamba ana imani kwamba rais Ruto atahudumu kwa mihula miwili.
Kwa upande wake Kimani Ichungwa ambaye ni mbunge wa Kikuyu na kiongozi wa walio wengi katika bunge la kitaifa alisema hatua ya Wezesha jamii ni njia moja wapo ya kufanikisha ajenda ya rais ya kuinua mwananchi wa chini.
“Hii mambo ya Empowerment mnaona tukifanya ni moja wapo ya ajenda na ahadi ya rais William Ruto katika mpango mzima wa Bottom Up, huyo mama wa chini aweze kupata pesa ya kufanya biashara hivyo sisi tumeamua wapige kelele wasipige, waseme tunawahonga wakenya hiyo sio shida yetu sisi tunataka kuona yule mwananchi wa chini anafaidika ndani ya serikali ya Rais William Ruto”. Alisema Ichung’wah.

Wakaazi wa Taveta katika mkutano wa Wezesha jamii
Hata hivyo siasa za rais Ruto kuhudumu mihula miwili zilisheheni huku viongozi mbalimbali wakitoa hundi za fedha ili kufanikisha mradi huo wa Wezesha jamii.
Miongoni mwa viongozi ambao walihudhuria halfa hiyo ni pamoja na Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula, Spika wa bunge la Seneti Amason Jeffa Kingi, Waziri wa michezo Salim Mvurya, Waziri wa madini na raslimali za baharini Ali Hassan Joho.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

