News
KMPDU yaonya madaktari wazembe pwani
Muungano wa madaktari nchini KMPDU tawi la pwani umeonya madaktari wazembe ukisema hautamtetea daktari yeyote atakayepatikana anakwepa majukumu yake.
Hii ni baada ya taarifa ya kamati ya afya ya bunge la seneti katika ziara yao kwenye hospitali ya rufaa ya Kilifi, kudai walikosa kuwaona baadhi ya madaktari waliopaswa kuwa kazini wakati huo.
Mwenyekiti wa KMPDU eneo la Pwani Daktari Niko Gichana alisema usimamizi wa kaunti unafaa kueleza chanzo cha madaktari hao kutokuwa kazini.
Gichana aliongeza kuwa hospitali za umma zinakumbwa na uhaba mkubwa wa madaktari na kusababisha waliopo kufanya kazi kwa mda mrefu bila mapumziko.
Afisa huyo alishauri usimamizi wa kaunti ya Kilifi kushughulikia suala la uajiri wa madaktari zaidi.
Kamati hiyo ikiongozwa na seneta David Wakoli Wafula ilibaini kuwepo dawa za matibabu zilizopitwa na wakati, baadhi ya madaktari kutofika kazini pamoja na hali duni ya usafi hospitalini wakati ilipozuru taasisi hiyo ya afya.
Ilimtaka gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro kuwachukulia hatua za kinidhamu wahudumu wa afya waliokwepwa majukumu.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

