Connect with us

News

KNCHR yatoa idadi ya waliofariki kwenye maandamano

Published

on

Tume ya kitaifa ya kutetea haki za kibinadamu nchini KNCHR imesema watu 8 wamethibitishwa kuaga dunia wakati wa maandamano yaliofanyika katika maeneo mbalimbali nchini.

Tume hiyo ilisema watu hao walifariki baada ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi katika maandamano ya kuwaenzi vijana wa Gen Z waliofariki wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha wa mwaka wa 2024, mwezi Juni 25, mwaka jana 2024.

KNCHR ilisema watu hao waliofariki ni kutoka kaunti 6 tofauti ambapo watu 2 kutoka kaunti ya Machakos, wawili kaunti ya Makueni, mmoja kaunti ya Nakuru, mmoja kaunti ya Kiambu, mmoja kaunti Uasin Gishu na mwengine katika kaunti ya Nyandarua.

Tume hiyo pia ilidokeza kwamba watu 400 walijeruhiwa katika maandamano hayo miongoni mwao ikiwa ni wanahabari, waandamanaji na maafisa wa polisi huku ikisema wengi wao ni wale waliokuwa wanahitaji matibabu ya dharura.

Hata hivyo tume hiyo iliweka wazi kwamba kuna baadhi ya watu ambao walikamatwa na kuzuiliwa na maafisa wa polisi, na hawapo katika vituo vya polisi huku ikikashifu vikali hatua ya mamlaka ya mawasiliano nchini CA, kwa kuzima mawimbi ya vituo vya habari nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending