Connect with us

Business

KPA kuanzisha ofisi ya uhusiano Kigali, Rwanda

Published

on

Serikali ya Kenya na Rwanda zimesaini mkataba wa makubaliano (MoU) unaolenga kuanza rasmi utekelezaji wa ofisi ya uhusiano ya halmashauri ya bandari nchini (KPA) jijini Kigali, Rwanda.

Hafla hiyo imeongozwa na katibu Mkuu wa idara ya uchukuzi nchini Mohamed Daghar, pamoja na katibu mkuu wa wizara ya miundombinu nchini Rwanda, CPA Canoth Manishimwe.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Daghar alisema makubaliano hayo yanaashiria dhamira ya pamoja ya nchi hizo mbili, kuimarisha ushirikiano wa kikanda, biashara na nafasi yao kimkakati katika sekta ya usafirishaji wa mizigo baharini na nchi kavu Afrika Mashariki.

Kwa upande wake, katibu mkuu wa Rwanda CPA Manishimwe alisema KPA ina mchango mkubwa katika kurahisisha biashara ya kikanda na kusaidia wafanyabiashara wa Rwanda na kwamba kuanzishwa kwa ofisi ya KPA Kigali kutarahisisha na kupunguza gharama za kutoa mizigo, huku wateja wakiweza kufanya taratibu nyingi wakiwa majumbani mwao.

Mkurugenzi Mkuu wa halmashauri ya bandari nchini KPA nahodha William Ruto, alisisitiza juhudi zinazoendelea za kuboresha shughuli za bandari, kuongeza uwezo na kuimarisha utoaji wa huduma akisema Rwanda inaendelea kuwa mojawapo ya masoko makubwa ya mizigo inayopita katika Bandari ya Mombasa, ambapo mwaka 2025 soko hilo lilikua kwa asilimia 22 sawa na tani 156,107.

Taarifa ya mwanahabari wetu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyibiashara wa mitumba eneo la Diani wafunga biashara zao

Published

on

By

Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Diani, kaunti ya Kwale, wamelazimika kufunga biashara zao kutokana na kudorora kwa shughuli za kibiashara katika kipindi hiki cha msimu wa watalii wachache na mvua zinazoendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.

Wafanyabiashara hao wanasema idadi ya wanunuzi imepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosababisha nguo nyingi kukosa soko.

Kulingana na wafanyibiashara hao wanategemea zaidi watalii wa ndani na nje  na kutokana na msimu huu kuwa uko uko chini wateja wamepungua hali inayofanya maisha kuwa mgumu.

Wanasema  wamelazimika kutupa baadhi ya nguo kwani  zimesalia sokoni kwa  muda mrefu hadi zingingine kuharibika, jambo ambalo limepelekea kupata hasara kubwa.

Aidha, wameongeza kuwa bei ya nguo za mitumba imeendelea kupanda ambapo wananunua ngunia moja kwa shilingi elfu 40 huku mauzo yakizidi kushuka.

“ Biashara imedorora sai kwani hakuna wateja ikizingatiwa kuwa tunategemea sana watalii na sasa hakuna wageni hata imetulazimu kutupa nguo kwani ngigi zimeharibika baada ya kukaa kwa mda mrefu bila kununuliwa”.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho

Published

on

By

Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.

Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.

Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.

Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.

Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.

“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending