Connect with us

Business

KPA kuanzisha ofisi ya uhusiano Kigali, Rwanda

Published

on

Serikali ya Kenya na Rwanda zimesaini mkataba wa makubaliano (MoU) unaolenga kuanza rasmi utekelezaji wa ofisi ya uhusiano ya halmashauri ya bandari nchini (KPA) jijini Kigali, Rwanda.

Hafla hiyo imeongozwa na katibu Mkuu wa idara ya uchukuzi nchini Mohamed Daghar, pamoja na katibu mkuu wa wizara ya miundombinu nchini Rwanda, CPA Canoth Manishimwe.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Daghar alisema makubaliano hayo yanaashiria dhamira ya pamoja ya nchi hizo mbili, kuimarisha ushirikiano wa kikanda, biashara na nafasi yao kimkakati katika sekta ya usafirishaji wa mizigo baharini na nchi kavu Afrika Mashariki.

Kwa upande wake, katibu mkuu wa Rwanda CPA Manishimwe alisema KPA ina mchango mkubwa katika kurahisisha biashara ya kikanda na kusaidia wafanyabiashara wa Rwanda na kwamba kuanzishwa kwa ofisi ya KPA Kigali kutarahisisha na kupunguza gharama za kutoa mizigo, huku wateja wakiweza kufanya taratibu nyingi wakiwa majumbani mwao.

Mkurugenzi Mkuu wa halmashauri ya bandari nchini KPA nahodha William Ruto, alisisitiza juhudi zinazoendelea za kuboresha shughuli za bandari, kuongeza uwezo na kuimarisha utoaji wa huduma akisema Rwanda inaendelea kuwa mojawapo ya masoko makubwa ya mizigo inayopita katika Bandari ya Mombasa, ambapo mwaka 2025 soko hilo lilikua kwa asilimia 22 sawa na tani 156,107.

Taarifa ya mwanahabari wetu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa

Published

on

By

Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.

Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.

Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Business

Wakulima wa Mananasi Magarini walilia soko

Published

on

By

Wakulima wa matunda aina ya nanasi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi wanaitaka serikali kuwatafutia soko ili kuuza bidhaa zao ambazo zinaendelea kuharibika msimu huu.

Kulingana na wakulima hao hakuna soko ambapo wanaweza kuuza bidhaa hizo kwa bei nzuri hali inayofanya wakulima wengi kuuza kwa bei ya chini ili kuepuka kuharibika kwa katunda hayo.

Wakizunumza na cocofm wakulima hao walisema kuwa kwa sasa wanakadiria hasara kwani matunda ni mengi.

Wakati huo huo wakulima hao wameitaka serikali ya kaunti kujenga viwanda.

Ni kauli ambayo imeongwa mkono na wafanyibiashara wa matunda mjini Kilifi kaunti ya Kilifi ambao walisema kuwa matunda mengi msimu huu huharibika kutokana na idadi ndogo ya wateja.

“Serikali itutafutie soko pamoja na kujenga viwanda ili kusaidia wakulima na wafanyibiashara wa matunda aina ya mamanasi, kuuza matunda yao ili kuawaepushia hasara hasa wakati huu ambapo matunda ni mengi.”

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending