Connect with us

News

Swazuri afikishwa Mahakamani kwa tuhma za ufisadi

Published

on

Mahakama ya kuu jijini Nairobi imesikiliza kesi ya ufisadi inayomkabili aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya kitaifa ya Ardhi (NLC), Prof Mohammad Swazuri, pamoja na washukiwa wengine 16.

Upande wa mashtaka umekuwa na nafasi ya kumhoji Swazuri kuhusu sakata ya ufisadi ya ulipaji fidia kwa waathiriwa wa mradi wa reli ya kisasa SGR wakati akiwa Mwenyekiti wa Tume hiyo.

Swazuri pamoja na wenzake 16 wanadaiwa kupanga njama ya kutekeleza ufisadi wa takriban shilingi milioni 220, fedha ambazo zilitengwa kulipa fidia waathiriwa wa mradi wa SGR ili ardhi zao zichukuliwe kwa ajali ya mradi huo.

Kulingana na uchunguzi uliyofanywa na idara ya upelelezi na kuwasilishwa Mahakamani, ulibaini kwamba kampuni binafsi ya Dasahe Investments na Olomotit Estate Limited, zililipwa fidia kwa njia isiyo halali licha ya madai kuwa ardhi husika ilikuwa mali ya umma.

Akijitetea mbele ya Hakimu Mkuu Mwandamizi Eunice Nyutu, Swazuri alijitenga na sakata hiyo akidai kwamba ni shtuma anazoelekezewa ni njama za kumchafulia jina na kumsambaratisha kisiasa, akiweka wazi kwamba hajawahi husika na sakata hiyo ya ufisadi.

Kesi hiyo itaendelea siku ya Ijumaa katika Mahakama hiyo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Baraza la Jamii ya Sekuye lalamikia uchimbaji wa madini kiholela

Published

on

By

Baraza la Wazee wa jamii ya Sekuye eneo la Moyale kaunti ya Marsabit limejitokeza na kulalamikia kuharibiwa kwa mazingira ya maeneo yao hasa katika kijiji cha Dabel kutokana na uchimbaji madini kiholela.

Wazee hao wamewalaumu viongozi wao ikiwemo serikali ya kaunti kwa kulinyamazia suala hilo huku wakaazi wakiendelea kunyanyaswa raslimali zao.

Baraza hilo, chini ya Katibu wake mkuu Haji Hassan Tepo, limedai kwamba uchimbaji huo wa madini kiholela, unyakuzi wa ardhi, unyanyasaji wa jamii umechangiwa na baadhi ya wawekezaji kutoka taifa Jirani la Somalia na Ethiopia ambao hawana vibali halali.

Hassan aliimtaka serikali kupitia Waziri wa madini nchini Hassan Ali Joho kuingilia kati suala hilo na kuhakikisha uchumbaji wa madini katika kijiji cha Dabel unasitishwa kwani wawekezaji zaidi ya 20 wamebuni makundi na kuendelea kuwanyanyasa wenyeji.

Hassan aliweka wazi kwamba baraza hilo pamoja na jamii ya Sekuye linapinga mpango huo na kusisitisha kwamba hawatakubali ardhi yao wanayoitegemea kwa shughuli mbalimbali kutumika vibaya.

Naibu Mwenyekiti wa baraza hilo Abdukadir Dilo alisema hali hiyo imewasabibishia hasara kwani mifugo imeangamia, uchumi wa kijiji hicho ukididimia zaidi na akamtaka rais Ruto kuingilia kati kwani licha ya Waziri Murkomen kufunga uchumbaji kufuatia utovu wa usalama bado wawekezaji kutoka Ethiopia na Somali wamekuwa wakiendeleza mpango huo.

Wazee hao hata hivyo walisisitiza kwamba hawatakubali kuachilia ardhi yao kunyakuliwa na watu wanaodai kuwa wawekezaji ilhali vijana wa eneo hilo hawana kazi, huku wanafunzi wakiacha shule na zaidi ya akina mama 22 wakiachwa na wanaume zao kufuatia suala hilo katika kijiji cha Dabel.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Murkomen ahimiza ushirikiano wa pamoja na wadau wa masuala ya ubaharia

Published

on

By

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen, ametoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya washirika na wadau ili kuimarisha usalama wa baharini na maziwa makuu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa kongamano la kamati ya uongozi wa Jukwaa la ushirikiano wa taarifa ya kanda ya Indo-Pasifiki (IORIS) lililofanyika mjini Mombasa, Waziri huyo alisisitiza kuwa ushirikiano wa mapema ni muhimu katika kukabiliana na vitisho vinavyoibuka vya usalama wa baharini.

“Ushirikiano wa mapema na muhimu katika kulinda usalama wetu wa baharini,” alisema Murkomen.

Kongamano hilo la siku tatu linaandaliwa kwa pamoja na huduma ya Walinzi wa Pwani ya Kenya (KCGS) pamoja na mradi wa njia muhimu za baharini wa Indo-Pasifiki unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU-CRIMARIO), ukiwaleta pamoja wadau wa usalama wa baharini..

Mradi wa EU-CRIMARIO umeundwa kuimarisha usalama na ulinzi wa baharini kupitia kuboreshwa kwa ushirikiano wa taarifa na uratibu wa operesheni.

Kongamano la siku tatu la kamati ya uongozi la Jukwaa la ushirikiano wa taarifa ya kanda ya Indo-Pasifiki (IORIS), Mombasa

Mpango wake mkuu, IORIS, ni jukwaa salama na lisiloegemea upande wowote linalotumia mtandao, unaounganisha zaidi ya mashirika 150 kutoka nchi 70, na kuwezesha uratibu wa operesheni za baharini kwa wakati halisi.

Kauli za Murkomen ilijiri kufuatia tangazo la Rais William Ruto kwamba kampuni ya usafiri wa baharini ya Norway, Wilhelmsen, itaajiri mabaharia 1,000 kutoka Kenya, baada ya mazungumzo na kampuni hiyo.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mkurugenzi wa EU-CRIMARIO Martin Cauchi Inglott, Mkurugenzi mkuu wa huduma ya walinzi wa Pwani ya Kenya Bruno Shioso, Naibu mkuu wa ujumbe wa umoja wa Ulaya nchini Kenya Ondrej Simek, pamoja na washkadau wengine.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending