News
KUPPET na KNUT washinikiza nyongeza ya mshahara
Chama cha Walimu wa shule za upili na vyuo vya kadri nchini KUPPET, kimeionya Tume ya uajiri walimu nchini TSC dhidi ya kuwasilisha pendekezo lipya linalokinzana na mkataba wa makubaliano wa malipo wa CBA wa mwaka wa 2025-2029.
Katibu mkuu wa KUPPET nchini, Akello Misori alisisitiza kwamba kuna haja ya kutathiminiwa upya kwa marupurupu yote ya walimu, akisema ni lazima mkataba huo unaangaliwe.
Akello alisema ili kuwawezesha walimu kutekeleza makujumu yao vyema, ni lazima serikali kupitia Tume ya kuajiri walimu nchini TSC kuangalia upya mkataba uliopo mezani na kuhakikisha matakwa ya walimu yanatekelezwa.
“Hivi karibuni kutatua na mazungumzo na muajiri wetu na sisi tuko na msimamo kwamba ni lazima nyongeza ya mshahara ya asilimia 50 na marupurupu ya walimu wanaofanyakazi katika mazingira magumu ya asilimia 30 pia iangaliwe upya”, alisema Akello.
Hata hivyo katika hafla tofauti, Naibu Mwenyekiti wa kitaifa wa chama cha walimu nchini KNUT Aggrey Namisi alisema iwapo hakutakuwa na mwafaka wowote kuhusu pendekezo hilo la CBA basi wataitisha mgomo wa kitaifa kuanzia mwezi Agosti.
“Sisi tuko tayari kufanya kazi lakini pia matakwa yetu ni lazima yaangaziwe na tunaiambia TSC kama itaendelea kugairi mambo yetu ya CBA mpya tutaambia walimu waanze mgomo mwezi Agosti na watakaoumia na wanafunzi wa gredi ya 9”, alisema Namisi.

Katibu mkuu wa KNUT Collins Oyoo
KUPPET na KNUT hata hivyo wanalenga kuweka mezani mahitaji mapya ya walimu wakati wa mazungumzo kati ya serikali na viongozi wakuu wa vyama hivyo huku suala la nyongeza ya mishahara na marupurupu ya asilimia 50 likipewa kipau mbele.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

